Kampuni ya STAMIGOLD ambayo ni kampuni tanzu ya Shirika la Madini la Taifa (STAMICO) kupitia mgodi wake wa Biharamulo uliopo wilayani Biharamulo mkoa wa Kagera umekabidhi  msaada wa  umeme wa jua kwa Kituo cha Polisi Mavota wenye thamani ya shilingi milioni 10/- za kitanzania lengo likiwa kuboresha mazingira ya  kazi katika kituo yatakayosaidia kuimarisha  ulinzi.

Msaada huo umekabidhiwa kwa Mkuu wa Kituo cha Polisi Mavota OCS. Bwana Antony Ramwa na Meneja Mkuu wa Mgodi wa Biharamulo Mhandisi Dennis Sebugwao.

Akizungumza katika hafla ya makabidhiano iliyofanyika jana katika Kituo cha Polisi Mavota kilichopo katika kijiji cha Mavota takribani kilomita tano kutoka lango kuu la mgodi Mhandisi Sebugwao alisema kuwa msaada wa umeme wa jua uliokabidhiwa ni utekelezaji wa mipango iliyowekwa na kampuni ya kuwezesha uwepo wa mazingira bora katika huduma za kijamii zikiwemo elimu, afya, maji na miundo mbinu hasa katika jamii zilizo jirani na mgodi
Meneja Mkuu wa mgodi wa Biharamulo Mhandisi Dennis Sebugwao (mwenye sare ya mgodi) akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya kukabidhi msaada wa umeme wa jua kwa Mkuu wa Kituo cha Polisi Mavota OCS Bwana Ramwa mwenye sare za Polisi (aliyeshika kifimbo).

 “Mgodi unatambua umuhimu wa kuwa na mazingira bora katika huduma za kijamii ikiwa ni pamoja na uwepo wa miundo mbinu itakayowezesha  wananchi kupata huduma muhimu bila vikwazo na ndio sababu Stamigold tukaona ni vyema kuweka umeme wa jua katika Kituo cha Polisi Mavota ili wananchi waweze kunufaika na huduma zitolewazo hata nyakati za usiku ukizingatia kituo hiki ni kituo pekee cha polisi katika kata nzima ya Kaniha ambapo kinahudumia takribani vijiji vitano” Alisema Sebugwao.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...