Kupitia mradi wa Airtel fursa ambao umekuwa ukitoa msaada mbalimbali kwa vijana nchini kwa kuwawezesha kufanikisha ndoto zao mmoja kati ya kijana anaejihusisha na ubunifu wa sanaa za uchoraji aliyenufaika na mradi huo Bi Theresia Maliatabu leo amemtembelea mkurugenzi mkuu wa Airtel na kumkabidhi picha yake aliyoichora mara tu airtel Fursa kumpatia Kijana huyo vifaa vya kidigital katika semina iliyofanyika miezi miwili iliyopita na kuchagua vijana wawili walioweza kuwezeshwa kwa kupatiwa vitendea kazi katika semina hiyo kwaajili ya kuboresha ubunifu wao.

Akikabidhi zawadi hiyo Theresia alisema” vifaa hivyo vinanisaidia kubuni baadhi ya michoro ambayo ni ya kisasa zaidi, lakini hasa inanisaidia mazoezi katika kuchora na vile vile inanisaida kama sehemu ya kutangaza biashara yangu kupitia social media”.

“Napenda kuwaambia vijana wenzangu kwamba wajiamini na vipaji walivyokuwa nazo wasikate tamaa kwani kila kitu kinawezekana na wasiache kuchangamkia fursa kama hizi zinapojitokeza, aliongeza Theresia

Mpaka sasa Airtel imefanya semina nyingi sana za mafunzo ya biashara ya ujasiriamli hapa nchini katika mikoa mbali mbali na kuweza kufikia vijana wapatao 4000. Airtel kupitia mpango wake wa Airtel FURSA utaendelea kutoa warsha hizi katika maeneo mbalimbali hapa nchini ili kuhakikisha inafikia vijana wengi zaidi. Vijana wanahamasishwa wanaposikia nafasi kama hii popote walipo , kuchangamkia kwa kuhudhuria kwani elimu inayotolewa ni bure kabisa bila gharama yoyote.
Kijana mjasiriamali Theresia Maliatabu (Kulia) akimkabidhi picha aliyoichora kwa ubunifu wake Mkurugenzi Mkuu wa Airtel, Sunil Colaso (Kushoto) kama shukrani yake kwa Airtel baada ya kuwezeshwa kupitia mpango wa Airtel FURSA "Tunakuwezesha" kwa kupatiwa vifaa vya kuboresha biashara yake, akishuhudiwa na Meneja wa huduma za jamii wa Airtel, Hawa Bayumi (katikati). Makabidhiano hayo yalifanyika mbele ya mkutano wa mwezi wa wafanyakazi Airtel uliyofanyika katika ofisi za Airtel Makao makuu morocco jijini Dar es salaam.
Kijana Theresia Maliatabu mmoja kati ya kijana anaejihusisha na ubunifu wa sanaa za uchoraji aliyenufaika na mpango wa Airtel FURSA “Tunakuwezesha” akiongea na wafanyakazi wa Airtel (hawapo pichani ) alipofika kwenye ofisi za Airtel makao makuu kukabidhi picha yake aliyoichora baada ya airtel Fursa kumpatia Kijana huyo vifaa vya kidigital katika semina iliyofanyika miezi miwili iliyopita na kuchagua vijana wawili walioweza kuwezeshwa kwa kupatiwa vitendea kazi katika semina hiyo kwa ajili ya kuboresha kazi zao.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...