Mkurungezi Mkuu wa Marie Stopes Tanzania, Anil Tambay akizungumza jijini Dar es Salaam Juni 15, 2016 katika uzinduzi wa ripoti ya mashirika ya mashirika yasiyo ya kiserikali katika kufunga miradi uliyokuwa unafadhiliwa na watu wa Australia kupitia mpango unaojulikana kwa jina la Australia - Africa Community Engagement Scheme (AACES) Tanzania, utakaofikia mwishoni Juni 30, 2016. AACES ulikuwa ni mradi wa miaka mitano, wa ushirikiano baina ya serikali ya Australia na Mashirika kumi yasiyo ya kiserika nchini humo pamoja na washirika wao walioko barani Afrika. Mradi huu umekuwa ukitekelezwa katika nchi za Ethiopia, Ghana, Kenya, Malawi, Msumbiji, Rwanda, Afrika Kusini, Tanzania, Uganda, Zambia na Zimbabwe.
Picha zote na Cathbert Kajuna wa Kajunason Blog.
Mgeni rasmi katika uzinduzi huo wa ripoti Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya na Maendeleo Jinsia, Watoto na Wazee, Dk Mpoki Ulisubisya akiwakabidhi hati ya umiliki wa bajaji vijana walioweza kusimamia vyema mradi wa AACES wa Marie Stopes Tanzania. Pembeni (aliyeshika kipaza sauti) ni Mkurungezi Mkuu wa Marie Stopes Tanzania, Anil Tambay na Meneja wa mrasi huo wa Marie Stopes Bi. Lilian Charles. Makabidhiano hayo yalifanyika jijini Dar es Salaam Juni 15, 2016 katika uzinduzi wa ripoti ya mashirika ya mashirika yasiyo ya kiserikali katika kufunga mradi uliyokuwa unafadhiliwa na watu wa Australia kupitia mpango unaojulikana kwa jina la Australia - Africa Community Engagement Scheme (AACES) Tanzania, utakaofikia mwishoni Juni 30, 2016.
Mgeni rasmi katika uzinduzi huo wa ripoti Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya na Maendeleo Jinsia, Watoto na Wazee, Dk Mpoki Ulisubisya (katikati) akioyesha ripoti mara aada ya kumaliza kuzindua.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...