Mfuko wa Pensheni wa PSPF leo hii umeanzisha rasmi mpango wa kukutana na wanachama wake na baadhi ya wajasiriamali jijini ili kupokea maoni na kuwahamasisha kujiunga na Mpango wa Uchangiaji wa Hiari (PSS) ili kunufaika na mafao mbalimbali yanayotolewa na mpango huo.

Akizungumza katika mkutano na wanachama na wajasiriamali kutoka soko la samaki la Feri Jijini Dar, Afisa Uendeshaji wa Mfuko wa Pensheni wa PSPF, Hadji Jamadary alisema kuwa mbali na kupokea maoni wanaendelea kutoa elimu ya juu ya mpango huo wa hiari ambapo mwanachama atakuwa huru kuchagua muda wa kuchangia kutegemea kipato chake huku kiwango cha chini kikianzia Shilingi 10,000 ambayo mwanachama anaweza kulipia kupitia benki na huduma za simu.

Bwana Hadji alisema kuwa mpango huo wa hiari unakaribisha raia na mtu asiye raia bila kusahau mjasiriamali na mfanyakazi wa serikali na kuongeza kuwa mwanachama anayejiunga katika mfuko huo huweza kupata mafao ya aina sita ambayo ni; Fao la Elimu, Fao la Ujasiriamali, Fao la Uzeeni, Fao la Kifo, Fao la Ugonjwa/Ulemavu, Fao la Kujitoa, na Fao la Matibabu.
Akifafanua kuhusu Fao la Matibabu, Bwana Hadji alisema kuwa kupitia mpango wake wa uchangiaji wa hiari wanashirikiana na mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF) ambapo mwanachama ataweza kupatiwa huduma bure katika hospitali na maduka ya madawa yaliyosajiliwa na NHIF kote nchini.

“Mwanachama anaweza kuwasajili pia wategemezi wake watano na kuendelea kupata mafao yetu bila shida yoyote,” alisema Hadji.

Wakizungumza kwa nyakati mbalimbali wajasiriamali hao walionesha kufurahia unafuu wa mfuko huo na kuwataka PSPF kuendelea kutoa elimu kwa jamii ili wananchi wengi wajiunge kwa kuwa hupoteza fedha nyingi ambazo wangeweza kuziokoa kwa kujiunga na mfuko huo.

Aidha Hadji aliwaambia wanachama hao kuwa PSPF ina mpango wa kuwawezesha wanachama wake na jamii kwa ujumla kumiliki nyumba zilizopo Dar , Morogoro, Tabora, Mtwara, Shinyanga na Iringa ambapo wataweza kununua kwa mkopo au malipo ya mara moja pamoja na mikopo ya viwanja vilivyo sehemu mbalimbali nchini.

Afisa Mwendeshaji kutoka Mfuko wa Pensheni wa PSPF Hadji Jamadary akiongea na wavuvi,Wafanyabiashara ya samaki pamoja na wajasiliamali waliopo katika soko la Samaki la Feri.
Katibu Kamati ndogo ya Utawala na Biashara Soko la Samaki la Feri Bw. Daudi Chiwinga akizungumza jambo wakati wa mkutano huo wa Mfuko wa Pensheni wa PSPF na wadau wake.
Afisa Mwendeshaji Msaidizi kutoka Mfuko wa Pensheni wa PSPF Nahshon Mshabaa akigawa fomu za kujiunga n NHIF kwa wadau wake wakati wa mkutano huo wa kupokea maoni na kuwaelimisha zaidi juu ya bidhaa za mfuko wa pensheni wa PSPF.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...