Familia ya Marehemu Mzee Gaspar Theodore Mtonga wa Majumba Sita Dar es Salaam (pichani) inayoheshima kutoa shukrani za dhati kabisa kwa ndugu, jamaa na marafiki ambao walishiriki kwa namna moja ama nyingine kufanikisha mazishi ya baba yetu mpendwa GASPAR THEODORE MTONGA aliyefariki dunia Mei 2, 2016 katika hospitali ya Hindu Mandal na Kuzikwa Matombo Morogoro Mei 6, 2016.


Kwa vile waliotuunga mkono na kutufariji wakati wa kipindi hiki kigumu  cha msiba ni wengi na ni vigumu kuwataja kwa majina. Familia, inapenda kwa heshima na taadhima nyingi kutoa shukrani za Jumla ikiwaomba kuzipokea shukrani hizo kwa moyo ule ule kama milivyo tuunga mkono.

Hata hivyo tunapenda kutoa shukrani za pekee kwa madaktari na wauguzi wote wa Hospitali ya Arafa iliyopo Majumba Sita na Hindul Mandal ya Dar es Salaam. Tunashukuru Uongozi wa SUMATRA Makao Makuu, Jeshi la Polisi Makao Makuu, Jeshi la Magereza Makao Makuu, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Morogoro,  Parokia ya Kipawa na Wanajumuia ya  Mtakatifu Maxmillian Kolbe Majumba Sita, Parokia ya Mtakatifu Paul Matombo ikiongozwa na Baba Paroko Amselm Kobelo na Wanakwaya wa Kanisa la Mtakatifu Paul Matombo. Majirani wote wa Majumba Sita na wa Kijiji cha Mwangazi Matombo waliofika kutufariji.
Tunawashukuru Sana. 
Mungu Awabariki.


Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...