Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda akizungumza katika mkutano wa wadau mawasiliano juu uzimwaji wa simu feki leo katika ukumbi wa Anatoglo jijini Dar es Salaam.
Sehemu ya wadau wa mawasiliano wakimsikiliza mkuu wa  mkoa hayupo pichani leo jijini Dar es Salaam.

Na Chalila Kibuda, Globu ya Jamii
Watanzania wametakiwa kutumia simu zenye viwango na kuachana simu bandia ambazo hata kiafya si salama kwa matumizi ya binadamu.

Hayo ameyasema leo Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda wakati mkutano wa wadau wa mawasiliano kuelekea uzimaji wa simu leo usiku wa kuamkia kesho, Makonda amesema TCRA imethubu kutoa huduma bora  kwa wananchi katika mawasiliano.

Amesema TCRA imeweza kupambana tangu uzimaji wa analojia kuingia digitali ambapo Tanzania imekuwa nchi ya mfano katika utekelezaji wa vitendo katika masuala mawasiliano.

Makonda amesema hata katika sheria ya mtandao baadhi ya watu walikuwa wanapinga ili kuweza kuendelea kutukana katika mitandao ambapo TCRA imeweza kufanikiwa kufanya hivyo.
Makonda amewataka wadau kuja na mawazo ya kuboresha huduma ya mawasiliano nchini katika ulinzi wa taifa.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...