Baadhi ya maofisa waandamizi wa Wizara ya Fedha na Mipango, wakiongozwa na Katibu Mkuu wa Wizara hiyo Dkt. Servacius Likwelile (aliyekaa kiti cha mbele), wakifuatilia mada iliyowasilishwa kwa wabunge kuhusu Marekebisho ya Sheria ya Ununuzi wa Umma, sura 410, katika ukumbi wa Pius Msekwa, Bungeni, Mjini Dodoma, jana
Kamishna wa Sera ya Ununuzi wa Umma, kutoka Wizara ya Fedha na Mipango, DKT. Fredrick Mwakibinga, akiwasilisha mada kwa waheshimiwa wabunge, kuhusu Marekebisho ya Sheria ya Ununuzi wa Umma, Sura 410, iliyofanyika katika ukumbi wa Pius Msekwa, Mjini Dodoma, jana.
Mbunge wa Nkasi, Ali Kessy, akichangia jambo wakati wa mjadala kuhusu Marekebisho ya Sheria ya Ununuzi wa Umma, Sura 410, wakati wa semina iliyofanyika katika ukumbi wa Pius Msekwa, Bungeni, Mjini Dodoma, Jana.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...