Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Nape Nnauye. akiwa katika mkao wa kusafisha kichwa unaojulikana kwa lugha ya Yoga "KAPALABHATI". Faifa za mkao huu ni pamoja na kusafisha njia za kupumulia na kuponya kukohoa, kutibu mafua, pumu na maambukizi kwa njiaya kupumua. Hali kadhalika unaufanya mwili kuchangamka na kuipa sura nuru na ujana na pia kustawisha mfumo wa neva na kuboresha mfumo wa kusaga chakula. Wazi Nape, ambaye alifuatana na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, aliongoza mamia ya wakazi wa jiji katika kuadhimisha Siku ya YogaDuniani kwenye ufukwe wa Coco Juni 19, 2016. (PICHA NA K-VIS MEDIA/KHALFAN SAID)
Mkao wa kusafisha kichwa (Kapalabhati).
Mkao unaosaidia mwili kuwa imara au kama unavyojulikana "Tadasana". Kutoka kushoto ni Wazir Nape, Balozi wa India nchini Tanzania, Sandeep Arya na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul makonda.
Umbo lapembe tatu au Trikonasana.
Yoga ikiendelea, kutoka kulia kwenda kushoto, ni aliyekuwa Balozi wa Tanzania nchini Uingereza, Peter Kalaghe, Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda, Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Nape Nnauye, Balozi wa India nchiniTanzania Sandeep Arya, na Balozi Mbelwa Kairuki.
BOFYA HAPA KWA PICHA ZAIDI
BOFYA HAPA KWA PICHA ZAIDI
Hizi imani zingine ni za Asia
ReplyDeleteKwani lazima kila kitu tuige jamani.
ReplyDeleteLol
Wabongo msifikiri kila kitu ni cha kuigwa, kuna mengine si mazuri kuigwa. Jitahidini kuheshimu mila na desturi za kitanzania / kiafrika.
ReplyDeleteYoga haina umuhimu wowote katika maisha yetu wabongo. Nyuma ya yoga kuna mengi yaliyojificha.
Yoga ni dini kamili, sasa wewe mbongo una dini yako, unaongeza dini nyingine ya nini?