Waziri wa Afya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Mhe Ummy Mwalimu (Mb.) amezitaka Halmashauri zote nchini kutoa vitambulisho kwa wazee waliopo katika Halmashauri zao. Haya ameyasema leo wakati akifungua Mkutano Mkuu wa mwaka wa Mtandao wa Mashirika ya Wazee, uliofanyika Mkoani Dodoma katika Ukumbi wa Maktaba Kuu ya Mkoa. 
Mheshimiwa Ummy Mwalimu (Mb.) Waziri wa Afya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto akiwa katika picha ya pamoja na wajumbe wa Mtandao wa Mashirika ya Wazee Tanzania.
Mheshimiwa Ummy Mwalimu (Mb.) Waziri wa Afya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto akihutubia wazee walioshiriki katika Mkutano Mkuu wa Mtandao wa Mashirika ya Wazee Tanzania
Akihutubia katika uzinduzi wa Mkutano huo Mheshimiwa Waziri Ummy alizitaka Halmashauri kuhakikisha wanatekeleza wajibu wao wa kutoa vitambulisho kwa wazee ili kuwezesha utambuzi wa wazee waliopo katika Halmashauri zao hususan katika utoaji huduma na mahitaji mbalimbali.

Mfano wa kitambulisho kinachotolewa kwa wazee wa Halmashauri ya Wilaya ya Kasuru.
Waziri Ummy alisisitiza kuwa Halmashauri zinatakiwa kutekeleza kwa vitendo kaulimbiu ya “Mzee Kwanza” hususan katika utoaji wa huduma za afya ambapo kila kituo cha Afya cha Umma kinatakiwa kiwe na chumba na watumishi maalum wa kuhudumia wazee. Pia ameziagiza Halmashauri zote nchini kuhakikisha wanakuwa na regista ya Wazee kwa kuainisha pia ujuzi wa wazee hao.
Mheshimiwa Waziri Ummy alieleza kuwa Serikali inatarajia kuwasilisha muswada wa sheria ya Wazee Bungeni Mwezi Septemba mwaka huu. Pia, aliwahakikishia wazee kuwa tatizo la upatikanaji wa dawa kwa wazee litapatiwa ufumbuzi kwa kiasi kikubwa kuanzia mwezi Julai 2016.

Mheshimiwa Ummy Mwalimu (Mb.) Waziri wa Afya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto akiwa katika picha ya pamoja na wajumbe wa Mtandao wa Mashirika ya Wazee Tanzania.

Mheshimiwa Ummy Mwalimu (Mb.) Waziri wa Afya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto akihutubia wazee walioshiriki katika Mkutano Mkuu wa Mtandao wa Mashirika ya Wazee Tanzania
Akihutubia katika uzinduzi wa Mkutano huo Mheshimiwa Waziri Ummy alizitaka Halmashauri kuhakikisha wanatekeleza wajibu wao wa kutoa vitambulisho kwa wazee ili kuwezesha utambuzi wa wazee waliopo katika Halmashauri zao hususan katika utoaji huduma na mahitaji mbalimbali.

Mfano wa kitambulisho kinachotolewa kwa wazee wa Halmashauri ya Wilaya ya Kasuru.
Waziri Ummy alisisitiza kuwa Halmashauri zinatakiwa kutekeleza kwa vitendo kaulimbiu ya “Mzee Kwanza” hususan katika utoaji wa huduma za afya ambapo kila kituo cha Afya cha Umma kinatakiwa kiwe na chumba na watumishi maalum wa kuhudumia wazee. Pia ameziagiza Halmashauri zote nchini kuhakikisha wanakuwa na regista ya Wazee kwa kuainisha pia ujuzi wa wazee hao.
Mheshimiwa Waziri Ummy alieleza kuwa Serikali inatarajia kuwasilisha muswada wa sheria ya Wazee Bungeni Mwezi Septemba mwaka huu. Pia, aliwahakikishia wazee kuwa tatizo la upatikanaji wa dawa kwa wazee litapatiwa ufumbuzi kwa kiasi kikubwa kuanzia mwezi Julai 2016.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...