Kampuni ya Tracto Co Ltd ni Wasambazaji rasmi wa Cummins Filtration ( Fleetguard ) na vilainishi vya Magari na Mitambo aina ya Valvoline nchini Tanzania.

Dhamira ni usambazaji wa bidhaa bora ili kuruhusu wasimamizi na wamiliki wa magari na mitambo kupunguza gharama za uendeshaji huku wakizingatia ubora. Timu ya wataalamu kwa kushirikiana na wataalamu kutoka Cummins na Valvoline hufanya kazi bega kwa bega na watumiaji wa mwisho wa bidhaa hizo kuhakikisha wanaitumia bidhaa kwa ufasaha na kuepuka majanga yatokanayo na utumiaji wa bidhaa hafifu. Utendaji umejengwa juu ya nguzo 4 ambazo ni:

Uchujaji/Filtration - Kuondoa Uchafu kutumia Bidhaa bora duniani kama - Fleetguard , MANN na PALL.

Vilainishi/Lubricants – Kampuni ya Tracto Co Ltd wanasambaza vilainishi bora kutoka Valvoline na Lubrication Engineers. Hivi ni vilainishi visivyokuwa na uchakachuaji wowote, wanakupa ubora uleule ulio pendekezwa na wazalishaji wa vyombo vyote vya moto.

Uhifadhi wa Mafuta – Hii hufanyika kwa kutumia matanki imara kabisa yaliyojengwa kwa kuta mbili, na huwekwa juu ya aridhi hivyo kurahisisha usafishaji na pia kurahisisha usafirishaji iwapo unataka kuhama, vivyo hivyo kuweza kugundua itilafu yoyote ikitokea katika tanki.

Uchunguzi na ufuatiliaji – Tunafanya Uchunguzi na Ukaguzi wa Mafuta kuona kiwango cha Usafi wake, na Kutoa ushauri kuhusu nini unatakiwa kukifanya kama mafuta yako tayari yana uchafu.
Afisa Mkuu wa Masoko ndg. Victor Ndamugoba akielezea bidhaa zao kwa watu waliofika kwenye banda lao (hawapo pichani).
Watu waliopata nafasi kutembelea banda la Tracto wakipata maelezo kutoka kwa wataalam kutoka Tracto.
Martin (mwenye nguo nyekundu) mtaalam wa vilainishi kutoka Valvoline akisiliza swali kwa makini kutoka kwa mmoja wa mteja aliyepita kutembelea banda la Tracto.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...