Na Chalila Kibuda, Globu ya Jamii.
Mbunge wa Mkuranga, Abdallah Ulega, amezindua ujenzi wa madarasa ya shule ya Msingi ya Mitawa,mwishoni mwa wiki,wilayani Mkuranga,Pwani,Ujenzi wa madara hayo unafuatiwa kutokana na shule ya hiyo kuwa na upungufu wa madarasa na kupelekea wanafunzi kusomea katika jengo la kupanga.
Akizungumza na wananchi wa Kitongoji cha Mitawa, Ulega amesema karne hii wanafunzi kusoma katika jengo la kupanga imepitwa na wakati, hivyo ni lazima wazazi wajitoe kujenga shule na serikali itatia mkono wake baada ya kuona njia ya kufanikisha jambo hilo.
Amesema suala linaloweza kufanya Taifa kuwa na maendeleo ni pamoja na kuwa wataalam ambapo lazima watoto waandaliwe katika mazingira ya shule na bila kufanya hivyo hakuna maendeleo hayo.Ulega amesema kama mbunge anawajibu wa kusimamia suala la elimu, kwa wananchi wa Mkuranga wanapata maendeleo ya elimu kwa kuwa na shule pamoja na walimu wa kutosha.
Katika ujenzi wa shule hiyo Mbunge amechangia zaidi ya milioni mbili na kuahidi kuendelea kutoa mchango mpaka pale shule itakapokamilika.Aidha amesema kufikia Januari shule hiyo imekamilika na wanafunzi waweze kuanza kusoma katika madarasa hayo na kuachana na kupanga jengo ambalo linatumika kwa sasa.
Mbunge wa mkuranga
akishiriki kufyatua matofali kwa ajili ya ujenzi wa darasa la shule ya msingi Mitawa pamoja na shughuli ya
ufyatuaji matofali Mbunge huyo pia alishiriki upandaji miti na kuzungumza na
wananchi,leo mkoani Pwani.
Mbunge wa Mkuranga, Abdallah Ulega, akizungumza na wananchi
wa Kitongoji cha Mitawa, Mkuranga juu ya maendeleo yaliyofikia katika Shule ya
Msingi Mitawa, leo.
Mbunge wa Mkuranga, Abdallah Ulega wapili (kutoka kushoto) akishiriki mazoezi na vijana wa Mkuranga leo
ikiwa ni sehemu ya kuwajenga vijana kuwa imara katika michezo.
Mbunge wa Mkuranga, Abdallah Ulega akizindua vyumba viwili
vya madarasa viliyojengwa na wananchi kwa kushirikiana na ofisi ya mbunge leo.Picha zote na Emmanuel
Massaka,Globu ya Jamii
Mbunge wa mkuranga
ashiriki ujenzi wa darasa la shule ya msingi Mitawa pamoja na shughuli ya
ufyatuaji matofali Mbunge huyo pia alishiriki upandaji miti na kuzungumza na
wananchi,leo mkoani Pwani.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...