Mkuu wa Wilaya ya Temeke  Mhe. Felix J. Lyaniva ametoa wito kwa Watanzania kujivunia bidhaa za Tanzania kupitia viwanda vyetu nchini, akisistiza kuwa Tanzania ina viwanda vinavyoweza kuzalisha bidhaa za kwetu na wananchi wajifunze kujivunia na kutumia bidhaa zetu wenyewe  ili kukuza uchumi wa viwanda.
Hayo ameyasema akiwa mgeni rasmi kwenye makabidhiano ya nyenzo za ushonaji kwa wasiiona wanaoendelea na mafunzo maalum ya ushonaji yanayoratibiwa na Mamlaka ya Maendeleo ya Biashara Tanzania (TanTrade).
Mhe Lyaniva aliongeza kwa kusema tarehe 7 hadi 11 Desemba katika viwanja vya Mwl. J.K Nyerere kutakuwa na Maonesho ya Viwanda vya Tanzania, na katoa wito kwa wananchi waje waone viwanda vya Tanzania na bidhaa zinazolishwa Tanzania wakiwemo wasioona wanaopata mafunzo maalum ili watambue uwezo wao wa ukuzaji wa uchumi wa viwanda.
Bw Shadrack Nkelebe, Meneja wa kiwanda cha nguo cha Urafiki amesema wamedhimiria kufanya kazi kwa karibu na Bw Abdallah Nyangalio anapoendelea kutoa mafunzo. Amesema  kwa nafasi yao ya uzalishaji wanavyo vitenge na khanga za kutosha  hivyo wanatoa ili kusaidia mafunzo maalumu ya ushonaji kwa wasioona maana kazi wanayofanya ni nzuri na yenye manufaa kwa taifa maana yanaleta maendeleo.
"Wakati wa maonesho ya Kimataifa ya Biashara Dar es Salaam (DITF) tulivutiwa sana na utendaji kazi wake lakini ni fundisho kwetu kwamba haya yanawezekana", alisema.
Nae Bw Abdallah Nyangalio mkufunzi na mlemavu wa macho wakati akipokea nyenzo hizo ameshukuru kupatiwa vifaa hivyo ambavyo vitamwezesha katika mafunzo yao na ana imani watafika mbali na kwamba tangu waanze mafunzo hayo tarehe 19 mwezi Oktoba, 2016 wanafunzi wamepiga hatua kubwa
Kaimu Mkurgenzi wa TanTrade Bw Edwin Rutageruka,  amemshukuru Mkuu wa Wilaya ya Temeke na Meneja Mkuu wa Kiwanda cha URAFIKI kwa msaada  wa nyenzo (Cherehani kutoka kwa Mkuu wa Wilaya na Majora kutoka Urafiki ) ambazo zitawasaidia katika mafunzo maalum ya ushonaji kwa wasiiona.
"Lengo la Mamlaka ya Maendeleo ya Biashara Tanzania ni kuhakikisha baada ya mafunzo hayo walemavu hawa wasioona watafutiwe na kupata masoko ya ndani na je ya nchi", alisema na kutoa wito kwa wananchi waje kuona kiwanda cha mlemavu asiyeona katika  kipindi hicho cha maonesho ya viwanda vya Tanzania maana atashiriki.  
 Mkuu wa Wilaya ya Temeke  Mhe. Felix J. Lyaniva akikakata utepe kama ishara ya kukabidhi msaada wa  cherehani kwa Bw.  Abdallah Nayngalio ambaye ni mkufunzi asiyeoona anayetoa  mafunzo maalum kwa ya ushonaji kwa wasioona yanayoratibiwa na Mamlaka ya  Maendelo ya  Biashara Tanzania (TanTrade). Kulia ni Bw Edwin Rutageruka, Kaimu Mkurgenzi wa TanTrade akifuatiwa na  Meneja Mkuu wa kiwanda cha URAFIKI  Bw Shadrack Nkelebe.
Mkuu wa Wilaya ya Temeke  Mhe. Felix J. Lyaniva akishuhudia Meneja Mkuu wa kiwanda cha nguo cha URAFIKI Bw Shadrack Nkelebe akimkabidhi majola ya vitenge kwa Bw Abdallah  Nyangalio ambaye ni mkufunzi asiyeoona anayetoa mafunzo  maalum ya ushonaji kwa wasioona yanayoratibwa na Mamlaka ya Maendeleo ya Biashara Tanzania (TanTrade). Kulia ni Bw Edwin Rutageruka, Kaimu Mkurgenzi wa TanTrade. Habari na picha na Theresa Chilambo wa TanTrade.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...