Na Antony John, Globu ya Jamii
Chama cha Wananchi Cuf kimethibitisha kushiriki uchaguzi mdogo ujao wa jimbo la Dimani visiwani humo.
Aizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo Mwenyekiti wa tume ya Taifa ya Uchaguzi Jaji Semistocles Kaijage, amesema kuwa chama hicho kitawakilishwa na mgombea wake Abdulrazak Khatibu Ramadhani katika uchaguzi mdogo wa jimbo la Dimani.
“Wagombea wengine ni Hamadi Mussa, ACT Wazalendo, Abdala Kombo khamis, chauma.Abdulazak Khatibu cuf Peter A. Magwira DP, Ali khamis Abdalla NRA. Sau Amour haji ali,SAU. TLP Pandu Haji Punda, UMD,Abdullsamad Salum Ali, UPDP,Bakari Omar.
Sambamba na hayo kaijage amesema kuwa kwa mujibu wa kifungu cha 31(1) b cha sheria ya Taifa ya uchaguzi sura ya 343 na kifungu cha 41( 1) vya sheria ya uchaguzi ya serikali yamitaa sura ya 292, tume imefanya uteuzi kwa wagombea wa ubunge na udiwani katika kata mbalimbali
Aidha ameongeza kuwa jumla ya vyama vyenye wagombea kwa jimbo la dimani Zanzibar ni 11 walioteuliwa kugombea ni 11 ambao wote ni wanaume kwa upande wa udiwani katika halmashauri 20 za Tanzania bara, vyama vyenye wagombea ni 13 jumla ya wagombea wa nafasi udiwani ni 72 kati ya wagombea hao wanawake ni 5 na wanaume ni67, hadi sasa pingamizi zilizokatwa ni sita ambapo tano ambapo tano zimekatwa kwenye kata ya ihumwa manispaa ya Dodoma na moja katika kata ya isegehe halmashauri ya mjini wa klahama.
Aliongeza kuwa kwa mujibu wa ratiba ya uchaguzi, kampeni zinaanza tarehe 23/12/2016 hadi 21/1/2016 ambapo kamati za maadili zitaundwa katika ngazi mbali mbali na zitakuwa na jukumu la kusimamia utekelezaji wa maadili katika kipindi chote cha kampeni.


Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...