Na Rhoda Ezekiel Buhigwe,

MKUU wa Wilaya ya Buhigwe Kanali Marko Gaguti amesema wameanza ziara ya siku 10 ya kutembelea na kukagua nyumba kwa nyumba  ili kuwabaini watu wanaonufaika na mpango wa kuwasaidia kaya masikini TASAF  awamu ya tatu,  ambao hawana sifa na kuwaondoa katika Mpango.

Katika ziara hiyo iliyoanza jana katika Kijiji cha Munanila,Dc Gaguti alisema katika Wilaya ya Buhigwe kuna jumla ya kaya 307 zilizo andikishwa kama kaya masikini, lakini hazina vigezo vya kunufaika na mradi huu kutokana na hali zao za kiuchumi na mazingira  wanayo ishi hayaonyeshi kuwa ni masikini hivyo watatakiwa kuondolewa katika mpango huo.

Alisema Ziara hiyo itafanyika kwa siku kumi itahusisha viongozi wote wa ngazi ya Kijiji,kata na Wilaya ili kuwabaini wale wote ambao hawastahili  waondolewe na wanufaika wabaki kuwa wale wanao stahili tuu kupatiwa msaada huo wa kaya lengwa.

Gaguti alisema kuna baadhi ya wanufaika wamekimbia baada ya kupewa taarifa ya uhakiki wa wanufaika wa mradi huo  kwa kuhofia wanaweza kutolewa,kwa wale ambao hawakuwepo kwenye kaya zao ili kuhakikiwa watakuwa wamejiondoa,kwa sasa tumetoa maelekezo kwa viongozi wa vijiji kushirikiana na serikali ili kukamilisha suala hilo kwa nakini bila kumpendelea wala kumuonea mtu yeyote.

"Leo tumeanza zoezi la kuwabaini wanufaika wasio na sifa zoezi,zoezi hili litakuwa ni la siku kumi katika ziara ya leo,na tumefanikiwa kuwabaini baadhi ya wanufaika ambao hawana sifa,hivyo watatakiwa kuondolewa kwenye mradi na kwa waliokwepa kufanyiwa tathimini ya kunufaika na mradi watakuwa wamejiondoa wenyewe, tunahitaji kubaki na watu ambao wana sifa ya kupatiwa fedha za TASAF ili lengo la serikali la kuzisaidia kaya masikini litimie",alisema Gaguti.
 
 MKUU wa Wilaya ya Buhigwe Kanali Marko Gaguti akizungumza na mmoja wa Wamufaika na mradi wa Kaya Masikini (TASAF),wakati wa ziara yake ya siku 10 ya kutembelea nyumba kwa nyumba  ili kuwabaini watu wanaonufaika na mpango wa kuwasaidia kaya masikini TASAF  awamu ya tatu,  ambao hawana sifa waondolewa katika Mpango.
 MKUU wa Wilaya ya Buhigwe Kanali Marko Gaguti akiwa sambamba na Mratibu wa TASAF Wilaya ya Buhigwe Chubwa Deogratius wakiendelea na ukaguzi wa Wamufaika na mradi wa Kaya Masikini (TASAF),wakati wa ziara yake ya siku 10 ya kutembelea nyumba kwa nyumba  ili kuwabaini wale watu wanaonufaika na mpango wa kuwasaidia kaya masikini TASAF  awamu ya tatu,bila kuwa na sifa  katika Mpango.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...