Na Veronica Simba - Makambako

Naibu Waziri wa Nishati na Madini, Dk Medard Kalemani ametoa ahadi kwa wakazi wa Kijiji cha Lyamkena kilichopo Makambako mkoani Njombe, kuwa watasherehekea sikukuu ya Krismas hapo Desemba 25 mwaka huu wakiwa na umeme. 

Dk Kalemani aliyasema hayo wakati akizungumza na wananchi husika jana kijijini hapo, mbele ya Mbunge wa Makambako Deo Sanga, akiwa katika ziara kukagua utekelezaji wa miradi mbalimbali ya umeme.Naibu Waziri alimwagiza Meneja anayesimamia Mradi wa Umeme wa Makambako – Songea, Didas Lyamuya, kuhakikisha kazi ya kutandaza nyaya inafanyika usiku na mchana ili umeme uwake katika eneo hilo kufikia Desemba 25.

“Tumekubaliana na Meneja, amejipanga kuanzia wiki ijayo wataanza kutandaza nyaya na watakamilisha ndani ya siku 10,” alifafanua.Aidha, Dk Kalemani alimwagiza Meneja huyo kuviingiza katika Mradi huo mkubwa wa umeme, vijiji vya Kihumba na Katani ambavyo vilisahaulika, ili vipatiwe umeme sambamba na maeneo mengine yote kama yalivyoainishwa katika Mradi.
Meneja wa Mradi wa Umeme wa Makambako – Songea, Didas Lyamuya (katikati), akifafanua jambo kwa Naibu Waziri wa Nishati na Madini, Dk Medard Kalemani (kulia) na Mbunge wa Makambako, Deo Sanga (kushoto), kuhusu maendeleo ya Mradi huo wakati wa ziara ya Naibu Waziri mkoani Njombe hivi karibuni
Naibu Waziri wa Nishati na Madini, Dk Medard Kalemani, akizungumza na wananchi wa Kijiji cha Lyamkena kilichopo Makambako mkoani Njombe hivi karibuni, wakati akiwa katika ziara kukagua miradi ya umeme.
Wananchi wa Kijiji cha Lyamkena, Wilaya ya Makambako mkoani Njombe, wakimsikiliza Naibu Waziri wa Nishati na Madini, Dk Medard Kalemani (hayupo pichani), wakati wa ziara yake mkoani humo hivi karibuni, kukagua miradi ya umeme.
Wananchi wa Kijiji cha Lyamkena, Wilaya ya Makambako mkoani Njombe, wakimsikiliza Naibu Waziri wa Nishati na Madini, Dk Medard Kalemani (hayupo pichani), wakati wa ziara yake mkoani humo hivi karibuni, kukagua miradi ya umeme.


Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...