Kocha wa mchezo wa masumbwi nchini, Rajabu Mhamila 'Super D' (kulia) akimnowa bondia Vicent Mbilinyi kwa ajili ya mpambano wake dhidi ya Mrisho Adamu, wa raundi kumi unaotarajiwa kufanyika Desemba 31, 2016 katika ukumbi wa Manyara Park, Jijini Dar es salaam.
Bondia Vicent Mbilinyi (kushoto) akionyeshana umwamba wa kutupiana makonde na Bondia Iddi Mkwela, wakati wa mazoezi yanayoendelea katika kambi ya Super D Coach Uhuru GYM, Kariakoo Jijini Dar es salaam. Mbilinyi anajiandaa na mpambano wake na dhidi ya Mrisho Adamu utakaofanyika Desemba 31 katika ukumbi wa Manyara Park Manzese, Jijini Dar es salaam.
Mabondia Iddi Mkwela (kushoto) na Vicent Mbilinyi wakioneshana umwamba wa kutupiana makonde. Picha na SUPER D BOXING NEWS
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...