Kaimu Kamishna Jenerali wa Magereza nchini, Dkt. Juma Malewa(wa pili kulia) akipokea vifaa vya michezo kutoka kwa Kaimu Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya SAN LAM Life Insurance, Bw. Samuel Mika(wa pili kushoto) ni Kamishna wa Fedha na Utawala wa Jeshi hilo, Kamishna Gaston Sanga(wa kwanza kushoto) ni Afisa Uhusiano wa Kampuni ya SAN LAM, Bw. Rishia Kileo. Vifaa hivyo vitatumiwa na Maafisa na Askari wa Jeshi la Magereza katika Mashindano ya Kijeshi yanayotarajiwa kufanyika Zanzibar mwezi huu Desemba, 2016.
 Kaimu Kamishna Jenerali wa Magereza nchini, Dkt. Juma Malewa akitoa neno la shukrani kwenye hafla fupi ya makabidhiano ya vifaa vya michezo vilivyotolewa na Kampuni ya SAN LAM Life Insurance. Hafla hiyo imefanyika leo Desemba 06, 2016 katika Ukumbi wa Makao Makuu ya Jeshi la Magereza, Jijini Dar es Salaam. Kushoto ni Kamishna wa Fedha na Utawala wa Jeshi hilo, Kamishna wa Magereza Gaston Sanga(kulia) ni Kaimu Mtendaji Mkuu wa Kampuni SAN LAM Life Insurance, Bw. Samuel Mika.
 Kaimu Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya SAN LAM Life Insurance, Bw. Samuel Mika akitoa maelezo mafupi kabla ya kukabidhi vifaa vya michezo kwa Jeshi la Magereza leo Desemba 06, 2016 katika Ukumbi wa Makao Makuu ya Jeshi la Magereza, Jijini Dar es Salaam.
 Mwenyekiti wa Kamati ya Michezo ya Jeshi la Magereza, SACP. Gideon Nkana akitoa utambulisho mfupi katika hafla ya kukabidhi vifaa vya michezo kwa Jeshi la Magereza leo Desemba 06, 2016 katika Ukumbi wa Makao Makuu ya Jeshi la Magereza, Jijini Dar es Salaam.
Kaimu Kamishna Jenerali wa Magereza Nchini, Dkt. Juma Malewa(katikati walioketi) akiwa katika picha ya pamoja na Maafisa Waandamizi wa Jeshi la Magereza pamoja na Wawakilikilishi wa Kampuni ya SAN LAM Life Insurance(waliosimama). hafla hiyo ya makabidhiano ya vifaa vya michezo imefanyika leo Desemba 06, 2016 katika Ukumbi wa Makao Makuu ya Jeshi la Magereza, Jijini Dar es Salaam.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...