Mgeni rasmi wakati wa fainali za Mahusiano Cup, katibu tawala wa wilaya ya Kahama Timoth Ndanya (Mwenye track suit nyekundu) akitoa mawaidha kwa wachezaji muda mfupi kabla ya kuanza kwa fainali za Mahusiano Cup
Katibu tawala wa wilaya ya Kahama Timoth Ndanya (Mwenye track suit nyekundu) akijianda kupiga mpira kuashiria kuanza kwa mchezo wa fainali ya Mahusiano Cup baina ya timu ya Kahama Mji na timu ya Mhungula.
Timu za netball za Kahama Mji na Zongomela zikionyeshana ufundi wa kucheza mpira wa pete wakati wa fainali za Mahusiano Cup kwa upande wa mpira wa pete. Timu ya Kahama mji iliibuka mshindi kwa kuwatandika wadogo zao wa Zongomela jumla ya vikapu 47 dhidi ya 24.
Wachezaji wa timu za Kahama Mji na Timu ya kata ya Mhungula wakiendelea na mchezo wa fainali za Mahusiano Cup mchezo ulioisha kwa timu ya Mhungula kuibuka kidedea kwa kuwachapa vijana wa mjini timu ya Kahama Mji jumla ya magoli matatu kwa mawili (3-2).

Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...