Hatimaye Makampuni matano yanayomilikiwa na Mfanyabiashara Yusuf Mehboub Manji yameondolewa katika Jengo la Quality Plaza linalomilikiwa na Shirika la Hifadhi ya Jamii la PSPF. Jengo hilo lipo Kitalu Na. 189/2 na liko mkabala na Barabara ya Nyerere jijini Dar es Salaam.

Sababu inayotajwa ya Makampuni hayo kuondolewa katika jengo hilo ni deni la kodi ya pango linalofikia kiasi cha Shilingi bilioni 13. Hatua ya kung'olewa makampuni hayo katika jengo hilo  ni baada ya mpangaji kushindwa kuondoka kwa hiari baada ya kupewa notisi ya masaa 24. 

Makampuni yaliyoondolewa ni Quality Group Company Limited, Gaming Management Limited, Q-Consult Limited, Quality Logistics Company Limited, na International Transit Investment Limited. Jeshi la Polisi lilisimamia wakati kampuni ya udalali ya Yono Auction Mart ikizihamisha kampuni hizo.

Inadaiwa kuwa Mfuko wa PSPF kwa muda mrefu umekuwa unaidai Kampuni ya Quality Group fedha hizo za upangaji, lakini kila inapotakiwa kulipa imekuwa ikikwepa na kukimbilia mahakamani kuweka pingamizi la kulipana kwamba uamuzi wa Mahakama Kuu uliotolewa Novemba 24, mwaka huu umemtaka aondoke ndani ya masaa 24 na kulipa deni analodaiwa.
Pia mmiliki wa kampuni hizo, japo amekwisha ondolewa katika jengo hilo amepewa muda wa siku 14 kisheria awe amelipa deni hilo na kama atashindwa kulipa mali zake zitakamatwa na kuuzwa ili kupata fedha za kulipa deni analodaiwa na PSPF.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...