Na Lydia Churi-Mahakama .
Jaji Mkuu wa Tanzania Mhe. Mohamed Chande Othman amewataka Mawakili nchini kuzingatia Maadili na kufuata misingi ya haki katika kutekeleza majukumu yao ili kesi ziendeshwe kwa haki, haraka na kwa wakati ili kuongeza imani ya wananchi kwa Mahakama.
Akizungumza wakati wa sherehe za kuwapokea na kuwaapisha Mawakili leo katika viwanja vya Karimjee jijini Dar es salaam, Jaji Mkuu amesema endapo Mawakili watatekeleza wajibu wao kwa kutenda haki watasaidia kupunguza mlundikano wa kesi zilizopo kwenye Mahakama mbalimbali nchini kuanzisha zile za Wilaya mpaka mahakama ya Rufani.
Aidha, Jaji Mkuu amewataka Mawakili kushirikiana Mahakama pamoja na wadau wengine katika kuutekeleza Mpango Mkakati wa miaka mitano wa Mahakama ya Tanzania ambao pamoja na mambo mengine pia unalenga kupunguza mlundikano wa kesi kwenye mahakama mbalimbali nchini.
Mhe. Othman pia amewashauri Mawakili walioapishwa leo kujiendeleza kielimu ili waweze kuongeza ujuzi utakaowasaidia kupambana na changamoto mbalimbali za kitaaluma na kwenda na wakati.
Jaji Mkuu wa Tanzania Mohamed Othman Chande akiongea mbele ya mawakili 258 hawapo pichani wakati wa sherehe ya 55 ya uhapisho huo iliyofanyika leo jijini Dar es salaam.
Jaji Mkuu wa Tanzania Mohamed Othman Chande katikati akiongoza Majaji wengine kupokea salamu ya utiifu kutoka kwa mawakili 258 waliopishwa hawapo pichani wakati wa sherehe ya 55 ya uhapisho huo iliyofanyika leo jijini Dar es salaam.
Baadhi ya Mawakili wakimsikiliza Jaji Mkuu wa Tanzania Mohamed Othman Chande hayupo pichani baada ya kuapishwa wakati wa sherehe ya 55 ya uhapisho huo iliyofanyika leo jijini Dar es salaam.
Baadhi ya Mawakili wakiwa wamesimama kusubiri kula kiapo kutoka kwa Jaji Mkuu wa Tanzania Mohamed Othman Chande wakati wa sherehe ya 55 ya uhapisho huo iliyofanyika leo jijini Dar es salaam.

Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...