Tuna furaha kubwa ya kuwaalika Watanzania wote wakazi wa mji wa Leicester UINGEREZA na vitongoji vyake kuhudhuria Mkutano wa Uzinduzi wa Jumuia ya Watanzania Leicester.
Lengo la Mkutano huo ni kuzindua Jumuia yetu, ambapo Masuala kadha yatajadiliwa, yakiwemo:
         Taratibu za kujiunga,   Umuhimu wa kuwa na Jumuia inayotambuliwa na Ubalozi pamoja na Serikali ya Tanzania,   Faida Za Kujiunga pamoja na thamani ya Diaspora kwa nchi ya Tanzania.

 Ushawishi wa kuunda Jumuia hii uliongezwa nguvu na Maofisa Ubalozi wa Tanzania UK mwaka jana: Walihimiza Haja ya Watanzania kujikusanya rasmi, lakini pia nia ya Serikali kushirikiana na Diaspora kujenga Tanzania ya sasa.
Ndugu zangu: UMOJA NI NGUVU!!
Katika kipindi hiki Mwaka Mmoja baada ya Uchaguzi Mkuu,
Wana Diaspora tuna maswali magumu yanayohitaji kujibiwa haraka!!!!
Tujikusanye, Tuwasilishe Changamoto zetu ili Tusikilizwe!!!
Jumuia ya watanzania Leicester itakuwa kiungo muhimu kati ya
Diaspora, Ubalozi na Serikali.

SIKU:     JUMAMOSI 17 DISEMBA 2016                   
MUDA:  SAA SABA KAMILI MCHANA   MPAKA SAA KUMI JIONI (1.00PM-4.00PM)
UKUMBI:   ST MATTHEWS CENTRE, 10 Malabar Road, Leicester, LE1 2PD
Tafadhali usikose Kuhudhuria
Tafadhali nawe tusaidie kualika wengine uwajuao. Shukrani sana!
Kwa Maelezo Zaidi wasiliana na MOSES KUSAMBA Simu:  07903 621150
Pia waweza kuwasiliana na Uongozi wa muda kwa E mail: tzumojaleicester@gmail.com

KARIBUNI NYOTE

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...