Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhandisi Ramo Makani (katikati)
akizungumza na watumishi wa Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro wilayani
Ngorongoro mkoani Arusha jana katika ziara yake ya kufuatilia utekelezaji
wa maagizo ya Waziri Mkuu. Kulia
ni Mhifadhi Mkuu wa Mamlaka hiyo, Freddy Manongi na Mbunge wa Jimbo la
Ngorongoro ambaye pia ni Naibu Waziri wa Kilimo, Mifugo na Uvuvi, William Ole
Nasha (kushoto). 
Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhandisi Ramo Makani (kulia)
akizungumza na watumishi wa Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro wilayani
Ngorongoro mkoani Arusha jana katika ziara yake ya kufuatilia utekelezaji wa
maagizo ya Waziri Mkuu, ametoa wiki mbili kwa watumishi wenye mifugo na
majengo ndani ya eneo la mamlaka ya hifadhi hiyo kujiandikisha kwa uongozi wa
mamlaka hiyo ikiwa ni mkakati wa utekelezaji wa maagizo ya Waziri Mkuu.
Naibu Waziri wa Kilimo, Mifugo na Uvuvi, William Ole
Nasha akichangia katika mkutano huo. Alieleza kuwa salama ya Hifadhi ya
Ngorongoro itategemea uwekaji wa mizania sawa baina ya uhifadhi na maendeleo ya
wananchi wa eneo hilo.
Mhifadhi Mkuu wa Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro,
Freddy Manongi (katikati) akizungmza katika mkutano huo. Kushoto ni Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhandisi Ramo Makani na Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Wanyamapori, Prof.
Alexandre Songorwa (kulia).
BOFYA HAPA KUSOMA HABARI KAMILI
BOFYA HAPA KUSOMA HABARI KAMILI
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...