Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira Mhe. Luhaga Mpina akimksikiliza Mkurungenzi wa Kituo cha Ujasiriamali Kutengeneza Nafasi za Kibiashara kwa Vijana Zanzibar Ndg, Ameir Sheha akitowa maelezo kwa Naibu Waziri alipowasili katika viwanja vya Kituo hicho huko Mbweni Zanzibar wakati wa ziara yake Zanzibar.
Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira Mhe. Luhaga Mpina akimsikiliza Mtaalamu Ufundi wa Kituo hicho Dr. Rajeev Aggrwal akitowa maelezo ya mafunzo kwa Vijana wanaojiunga na Kituo hicho kupata Elimu ya Ujasiriamali na baadae kujiajiri mwenyewe baada ya kupata ujenzi kupitia kituo hicho, kilioko katika majengo ya Chuo cha Karume Mbweni Zanzibar.
Naibu Waziri Ofisi wa Makamu wa Rais Muungano na Mazingira akipitia ripoti ya Kituo hicho baada ya kupata maelezo kutoka kwa Wataalamu wa Kituo hicho wakati wa ziara yake Zanzibar kutembelea Taasisi mbalimbali.
Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira Mhe. Mpina akiwa na Mkurugenzi Mkuu wa Kituo cha Kukuza Ujasiriamali Kutengeneza Nafasi za Kibiashara kwa Vijana Ndg. Ameir Sheha, akimtembeza katika Kituo hicho kujionea shughuli zinazofanywa kutowa mafunzo kwa Vijana wanaojiunga kupata mafunzo ya ujasiriamali.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...