Katibu wa Halmashauri Kuu, Itikadi na Uenezi, Nape Nnauye
KAMATI
Kuu (CC) ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) imekutana mjini Dar es Salaam na
kujadili ajenda moja ya kupokea tathmini ya Chama baada ya uchaguzi mkuu
wa Oktoba 25, mwaka jana.
Akizungumza na waandishi wa habari Ofisi Ndogo za Makao Makuu ya CCM, Lumumba Dar es Salaam, leo, Katibu wa Halmashauri Kuu, Itikadi na Uenezi, Nape Nnauye, alisema kikao hicho kilichoongozwa na Mwenyekiti wa CCM, Rais John Magufuli kilijadili tathmini hiyo kabla ya kupelekekwa mbele kulingana utaratibu wa Chama.
Nape Mbaye pia ni Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, alisema tathmini hiyo ilitokana na maagizo ya Chama kwenye ngazi zote kufanya tathmini hususan baada ya kumalizika kwa uchaguzi mkuu huo.Kwa mujibu wa Nape, huo ni utamaduni wa kawaida wa CCM kufanya tathmini kila baada ya uchaguzi ambayo imekuwa ikifanyika kwa maagizo ya Chama kuanzia ngazi ya tawi, kata, wilaya, mkoa na kuendelea.
Alisema Kamati Kuu itaipitia tathmini hiyo kisha itawasilisha mbele ya Halmashauri Kuu ya CCM ambako itajadiliwa na kuelekeza hatua zinazofuata."Hii ndio siri ya uimara na ushindi wa CCM. Tumekuwa tukijitathmini na kuchukua hatua stahili kwa ajili ya kuhakikisha Chama kinaendelea kuwa imara na bora siku zote,"alisema.
Aidha, alisma awali kikao hicho kilipangwa kufanyika kwa siku mbili lakini kilifanyika kwa siku moja na kwamba kilitarajiwa kukamilika jana.Nape alisema kikao cha Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC) ya CCM kilichopangwa kufanyika kesho kitafanyika kama kilivyopangwa ambapo alitumia fursa hiyo kuwatakia safari njema wajumbe wote wanaotoka sehemu mbalimbali za nchi kwa ajili ya kuhudhuria hicho.
Akizungumza na waandishi wa habari Ofisi Ndogo za Makao Makuu ya CCM, Lumumba Dar es Salaam, leo, Katibu wa Halmashauri Kuu, Itikadi na Uenezi, Nape Nnauye, alisema kikao hicho kilichoongozwa na Mwenyekiti wa CCM, Rais John Magufuli kilijadili tathmini hiyo kabla ya kupelekekwa mbele kulingana utaratibu wa Chama.
Nape Mbaye pia ni Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, alisema tathmini hiyo ilitokana na maagizo ya Chama kwenye ngazi zote kufanya tathmini hususan baada ya kumalizika kwa uchaguzi mkuu huo.Kwa mujibu wa Nape, huo ni utamaduni wa kawaida wa CCM kufanya tathmini kila baada ya uchaguzi ambayo imekuwa ikifanyika kwa maagizo ya Chama kuanzia ngazi ya tawi, kata, wilaya, mkoa na kuendelea.
Alisema Kamati Kuu itaipitia tathmini hiyo kisha itawasilisha mbele ya Halmashauri Kuu ya CCM ambako itajadiliwa na kuelekeza hatua zinazofuata."Hii ndio siri ya uimara na ushindi wa CCM. Tumekuwa tukijitathmini na kuchukua hatua stahili kwa ajili ya kuhakikisha Chama kinaendelea kuwa imara na bora siku zote,"alisema.
Aidha, alisma awali kikao hicho kilipangwa kufanyika kwa siku mbili lakini kilifanyika kwa siku moja na kwamba kilitarajiwa kukamilika jana.Nape alisema kikao cha Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC) ya CCM kilichopangwa kufanyika kesho kitafanyika kama kilivyopangwa ambapo alitumia fursa hiyo kuwatakia safari njema wajumbe wote wanaotoka sehemu mbalimbali za nchi kwa ajili ya kuhudhuria hicho.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...