Na. Aron Msigwa – NEC, Zanzibar.

Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) imevitaka Vyama vya Siasa na wagombea watakaoshiriki Uchaguzi mdogo katika jimbo la Dimani visiwani Zanzibar kuzingatia Sheria , Kanuni, Taratibu na Maadili ili Uchaguzi huo uwe huru na wa haki na kuwawezesha wananchi kuchagua viongozi wanaowataka.

Kauli hiyo imetolewa leo mjini Zanzibar na Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi Jaji Mstaafu Damiani Lubuva wakati akizungumza na Viongozi 19 wa vyama vya Siasa waliohudhuria mkutano wa maandalizi ya kufanikisha Uchaguzi mdogo wa jimbo la Dimani utakaofanyika Januari 22, 2017.

Amewataka viongozi wa Vyama vya Siasa waliohudhuria mkutano huo waendelee kudumisha hali ya amani na Utulivu wakati wa kampeni za vyama vyao zinazotarajiwa kuanza hivi karibuni pia kutoa ushirikiano kwa Waratibu na Wasimamizi wa Uchaguzi huo.

“Ni matarajio ya Tume kuwa, Vyama vya Siasa vitatoa ushirikiano wa hali ya juu ili kuhakikisha uchaguzi wetu katika jimbo la Dimani unakuwa Huru na wa Haki, lengo hili litafanikiwa tu iwapo vyama na wagombea wote watazingatia na kufuata sharia na maelekezo na maadili ya Tume” Amesisitiza Jaji Lubuva.

Amevitaka vyama vyote vitakavyoshiriki katika uchaguzi huo wakati wa kampeni vijikite katika kuelezea Sera zao na si vinginevyo pia kuepuka matumizi ya lugha ambazo zinaweza kusababisha machafuko.

Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi Jaji Mstaafu Damiani Lubuva akifungua kikao cha Tume ya Taifa ya Uchaguzi na vyama vya Siasa vitakavyoshiriki katika uchaguzi mdogo katika jimbo la Dimani Zanzibar leo.
Mkurugenzi wa Uchaguzi wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi Bw. Kailima Ramadhani akitoa ufafanuzi kwa viongozi wa vyama vya Siasa kuhusu maadili ya kuzingatia kwa vyama vya Siasa wakati wa uchaguzi huo na maandalizi ya Uchaguzi wa jimbo la Dimani leo mjini Zanzibar. 
Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi Jaji Mstaafu Damiani Lubuva (kushoto) akiwa na wajumbe wa NEC wakakifuatilia mkutano huo leo mjini Zanzibar.
Mkurugenzi wa Uchaguzi wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) Bw. Kailima Ramadhani akitoa ufafanuzi kwa viongozi wa vyama vya Siasa kuhusu maadili ya kuzingatia kwa vyama vya Siasa wakati wa uchaguzi huo na maandalizi ya Uchaguzi wa jimbo la Dimani leo mjini Zanzibar. 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...