Kaimu Balozi, Bi. Talha Mohamed Waziri (Kushoto) akisalimiana na Maskauti kutoka Tanzania.
Skauti 27 kutoka shule mbili za msingi za Dar es Salaam wako nchini Kenya kwa ziara ya wiki moja kwa mwaliko wa Chama cha Maskauti cha Kenya.
Watoto hao kutoka shule za msingi za Canossa na Libermann, na maofisa wa Chama cha Maskauti Tanzania waliowasindikiza, Kamishina Anthony Joachim na Kamishina Saidi Debwani, leo wametembelea Ubalozi wa Tanzania Nairobi na kusalimiana na Kaimu Balozi, Bi.Talha Mohamed Waziri.
Maskauti hao walimwambia Kaimu Balozi kuwa wametembelea maeneo mbalimbali ya Kenya na kujifunza mambo mengi.Kamishina Joachim amesema watoto hao wanatarajiwa kurejea nyumbani kesho.
Maskauti kutoka Tanzania na viongozi wao katika picha ya pamoja na Kaimu Balozi, Bi. Talha Mohamed Waziri.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...