Kaimu Balozi, Bi. Talha Mohamed  Waziri (Kushoto) akisalimiana na Maskauti kutoka Tanzania.

Skauti 27 kutoka shule mbili za msingi za Dar es Salaam wako nchini Kenya kwa ziara ya wiki moja kwa mwaliko wa Chama cha Maskauti cha Kenya.
Watoto hao kutoka shule za msingi za Canossa na Libermann, na maofisa wa Chama cha Maskauti Tanzania waliowasindikiza, Kamishina Anthony Joachim na Kamishina Saidi Debwani, leo wametembelea Ubalozi wa Tanzania Nairobi na kusalimiana na Kaimu Balozi, Bi.Talha Mohamed Waziri.

Maskauti hao walimwambia Kaimu Balozi kuwa wametembelea maeneo mbalimbali ya Kenya na kujifunza mambo mengi.Kamishina Joachim amesema watoto hao wanatarajiwa kurejea nyumbani kesho.
Maskauti kutoka Tanzania na viongozi wao katika picha ya pamoja na Kaimu Balozi, Bi. Talha Mohamed  Waziri.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...