Na Pascal Mayalla 
 Tanzania imeanza kutumia vizuri Mabilioni ya Taasisi ya TradeMark East Africa, kuwajengea uwezo wafanyabiashara wanawake wa Tanzania, kwa kugharimia mafunzo ya kuwajengea uwezo Wafanyabiashara Wanawake wa Tanzania, walio chini ya mwamvuli wa Chama cha Wafanyabiashara Wanawake Tanzania , (Tanzania Women Chamber of Commerce, TWCC), ili kuweza kuvuka mipaka na kuwezesha bidhaa za Tanzania, kuyafikia masoko ya nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki na hata nje ya bara la Afrika. 
 Akizungumzia kuanza kwa mafunzo hayo, Mkurugenzi wa TradeMark Tawi la Tanzania, Bw. John Ulanga, aliyewakilishwa na Program Manager wa TradeMark East Africa, Tawi la Tanzania, Bi Monica Hangi, amesema, mafunzo hayo ni sehemu ya utakelezaji wa mradi mkubwa wa Taasisi ya Trademark East Africa ujulikanao kama “Women in Trade” unaolenga kuwajengea uwezo wafanyabiashara wanawake wa Tanzania, kuhimili ushindani wa kibiashara na kukabiliana na vikwazo vya kibiashara kwa wafanyabiasha wanawake Tanzania kuwawezesha kufanya biashara ya kimataifa ikiwemo kuwezesha bidhaa zao kuyafikia masoko ya nchi za Afrika Mashariki na masoko ya kimataifa.
Taasisi ya TradeMark imetenga Dola za Marekani Milioni 5,300,000 ambazo ni zaidi ya Shilingi Bilioni 12 za Kitanzania kugharimia mpango huo. Bi Hangi amesema, “Ukimuwezesha mwanamke, ni kuiwezesha familia nzima, familia zikiwezeshwa ni kuwezesha jamii nzima na jamii zikiwezeshwa na kuwezesha taifa kwa ujumla, hivyo uwezeshaji huo kwa wanawake ni uwezeshaji kwa taifa kupata maendeleo” 
 Program Manager wa TradeMark East Africa, Tawi la Tanzania, Bi Monica Hangi, akitunuku cheti cha kuhitimu mafunzo ya kuvuka mipaka, kwa mjasiliamali wa Mavazi, Bi. Daria Gwao Makaramba kwenye hafla fupi  ya kufunga mafunzo ya kuwajengea uwezo wa kuvuka mipaka kwa wafanyabiashara wanawake  wa Tanzania yaliyoandaliwa na Chama cha Wafanyabiashara Wanawake Tanzania (TWCC) ili kuwezesha bidhaa za Tanzania, kuyafikia masoko ya Afrika Mashariki . Mafunzo hayo, yameendeshwa taasisi ya mafunzo ya CABO Consult na kufadhiliwa na TradeMark East Africa.
 Program Manager wa TradeMark East Africa, Tawi la Tanzania, Bi Monica Hangi, akitunuku cheti cha kuhitimu mafunzo ya kuvuka mipaka, kwa mjasiliamali wa kusindika vyakula, Mwal. Rose Romanus kwenye hafla fupi  ya kufunga mafunzo ya kuwajengea uwezo wa kuvuka mipaka kwa wafanyabiashara wanawake  wa Tanzania yaliyoandaliwa na Chama cha Wafanyabiashara Wanawake Tanzania (TWCC) ili kuwezesha bidhaa za Tanzania, kuyafikia masoko ya Afrika Mashariki . Mafunzo hayo, yameendeshwa taasisi ya mafunzo ya CABO Consult na kufadhiliwa na TradeMark East Africa.
 Program Manager wa TradeMark East Africa, Tawi la Tanzania, Bi Monica Hangi, akitunuku cheti cha kuhitimu mafunzo ya kuvuka mipaka, kwa mjasiliamali kijana, Hadija Ahmed, kwenye hafla fupi  ya kufunga mafunzo ya kuwajengea uwezo wa kuvuka mipaka kwa wafanyabiashara wanawake  wa Tanzania yaliyoandaliwa na Chama cha Wafanyabiashara Wanawake Tanzania (TWCC) ili kuwezesha bidhaa za Tanzania, kuyafikia masoko ya Afrika Mashariki . Mafunzo hayo, yameendeshwa taasisi ya mafunzo ya CABO Consult na kufadhiliwa na TradeMark East Africa.
 Washiriki wa mafunzo ya kuvuka mipaka, kwenye hafla fupi  ya kufunga mafunzo ya kuwajengea uwezo wa kuvuka mipaka kwa wafanyabiashara wanawake  wa Tanzania yaliyoandaliwa na Chama cha Wafanyabiashara Wanawake Tanzania (TWCC) ili kuwezesha bidhaa za Tanzania, kuyafikia masoko ya Afrika Mashariki . Mafunzo hayo, yameendeshwa taasisi ya mafunzo ya CABO Consult na kufadhiliwa na TradeMark East Africa.
Washiriki wa mafunzo ya kuvuka mipaka, kwenye picha ya pamoja na vyeti vyao baada ya kuhitimu mafunzo ya kuwajengea uwezo wa kuvuka mipaka kwa wafanyabiashara wanawake  wa Tanzania yaliyoandaliwa na Chama cha Wafanyabiashara Wanawake Tanzania (TWCC) ili kuwezesha bidhaa za Tanzania, kuyafikia masoko ya Afrika Mashariki . Mafunzo hayo, yameendeshwa taasisi ya mafunzo ya CABO Consult na kufadhiliwa na TradeMark East Africa.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...