Na Chalila Kibuda, Globu ya Jamii
MBUNGE wa Mkuranga Mhe. Abdallah Ulega amefanya ziara katika vijiji vya Kisayani na Msorwa ili kujua changamoto mbalimbali zinazowakabiliwa wananchi na kuweza kuzishughulikia kupitia Halmashauri pamoja Ofisi yake.
Akizungumza na wananchi waVijiji hivyo amesema wakati wa sasa ni kufanya wa maendeleo ya kweli bila kuangalia itikadi za vyama.
Amesema kwa kutambua umuhimu wananchi kuwa watu wako katika mapumziko ya sikukuu za mwisho wa mwaka lakini ameona bora kutembelea wananchi waliompigia kura. Ulega amesema Mkuranga inahitaji maendeleo kutokana na kukaa muda mrefu bila kuwa na mabadiliko ya wananchi katika huduma za jamii kutokana na viongozi
Amesema kazi yake ni kuhamasisha wananchi katika masuala ya maendeleo pamoja na kupokea na kusikiliza kero na changamoto mbalimbali za wanachi wa vijiji hivyo katika ziara hiyo, amepokea changamoto mbalimbali ikiwemo ubovu wa miundominu ya barabara, Afya,Elimu, Umeme pamoja na Maji ambapo amewahakikishia wananchi hao kuzishughulikia changamoto hizo zinazo wakabili ili kuchochea maendeleo ya vijiji hivyo.
Ulega amesema ameweza kufanya ziara katika vijiji 90 kati ya vijiji 125 katika Jimbo la Mkuranga ambapo kati ya vijiji hivyo asilimia 50 changamoto zimetatuliwa.
MBUNGE wa Mkuranga Mhe. Abdallah Ulega amefanya ziara katika vijiji vya Kisayani na Msorwa ili kujua changamoto mbalimbali zinazowakabiliwa wananchi na kuweza kuzishughulikia kupitia Halmashauri pamoja Ofisi yake.
Akizungumza na wananchi waVijiji hivyo amesema wakati wa sasa ni kufanya wa maendeleo ya kweli bila kuangalia itikadi za vyama.
Amesema kwa kutambua umuhimu wananchi kuwa watu wako katika mapumziko ya sikukuu za mwisho wa mwaka lakini ameona bora kutembelea wananchi waliompigia kura. Ulega amesema Mkuranga inahitaji maendeleo kutokana na kukaa muda mrefu bila kuwa na mabadiliko ya wananchi katika huduma za jamii kutokana na viongozi
Amesema kazi yake ni kuhamasisha wananchi katika masuala ya maendeleo pamoja na kupokea na kusikiliza kero na changamoto mbalimbali za wanachi wa vijiji hivyo katika ziara hiyo, amepokea changamoto mbalimbali ikiwemo ubovu wa miundominu ya barabara, Afya,Elimu, Umeme pamoja na Maji ambapo amewahakikishia wananchi hao kuzishughulikia changamoto hizo zinazo wakabili ili kuchochea maendeleo ya vijiji hivyo.
Ulega amesema ameweza kufanya ziara katika vijiji 90 kati ya vijiji 125 katika Jimbo la Mkuranga ambapo kati ya vijiji hivyo asilimia 50 changamoto zimetatuliwa.
Mbunge wa
Mkuranga, Mhe. Abdallah Ulega akizungumza na wananchi wa kijiji cha Kisayani
alipokwenda kuwatembelea pamoja na kuangalia maendeleo ya kijiji hicho
leo
Sehemu ya
wananchi wa kijiji cha Kisiyani wakimsikiliza Mbunge wa Mkuranga ,
Abdallah Ulega
Diwani wa
Kata ya Mbezi, Mkuranga, Rashid Selungwi akizungumza na wananchi wa Kijiji cha
Msorwa katika ziara ya Mbunge wa Mkuranga Abdallah Ulega leo.
Mkazi wa Kijiji
cha Kisiyani Kata ya Mbezi, Joel Kianga akichangia mada katika ziara ya Mbunge
wa Mkuranga, Abdallah Ulega leo.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...