Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Fedha na Mipango Bi. Doroth Mwanyika (kulia), akimsikiliza Kaimu Mkuu wa Chuo cha Uhasibu Arusha Dkt. Faraji Kasidi (kushoto) wakati akielezea mafanikio na changamoto zinazokikabili chuo hicho. Kushoto kwa Mkuu wa Chuo ni Mkaguzi wa Ndani Mkuu wa Serikali Bw. Mohamed Mtonga, Msaidizi wa Mkuu wa Chuo Dkt. Samwel Werema, Mkaguzi wa Ndani Mkuu Msaidizi– Ukaguzi Mamlaka za Mitaa Bw. Mwanyika Musa na Mkuu wa Kitengo cha Ukaguzi wa Kiufundi Bw. Amin Mcharo
Naibu Katibu Mkuu, Wizara ya Fedha na Mipango Bi. Doroth Mwanyika (kulia), akijibu hoja zilizotolewa na Kaimu Mkuu wa Chuo cha Uhasibu Arusha Dkt. Faraji Kasidi (kushoto) alipofika Ofisi Kuu ya Chuo hicho kabla ya kufungua mafunzo ya siku nne ya wakaguzi kutoka mikoa ya Kanda ya Kaskazini.
Kaimu Mkuu wa Chuo cha Uhasibu Arusha Dkt. Faraji Kasidi aliyesimama akitoa utangulizi kabla ya kumkaribisha mgeni rasmi katika ufunguzi wa mafunzo kwa wakaguzi wa Ndani kutoka Serikali za Mitaa na Sekretarieti za Mikoa. Kushoto kwake ni Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Fedha na Mipango Bi. Doroth Mwanyika, Mkaguzi wa Ndani Mkuu wa Serikali Mohamed Mtonga, Mkuu wa Kitengo cha Ukaguzi wa Kiufundi Bw. Amin Mcharo na kulia kwa Kaimu Mkuu wa Chuo ni Mkaguzi wa Ndani Mkuu Msaidizi wa Serikali – Ukaguzi mamlaka za mitaa Bw. Mwanyika Musa.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...