Na Jacquiline Mrisho – MAELEZO.
Aliyekuwa Mbunge wa Viti maalum (CCM), Mhe. Anna Abdallah amewataka wanawake nchini kuacha kusubiri nafasi za upendeleo wa nafasi za uongozi katika vyombo mbalimbali vya maamuzi nchini.

Mhe. Anna Abdallah ameyasema hayo leo jijini Dar es Salaam wakati wa mahojiano maalum juu ya maendeleo na nafasi ya wanawake katika nafasi za uongozi ndani ya miaka 55 tangu nchi yetu ipate Uhuru wake mwaka 1961.
Amesema kuwa, katika miaka ya nyuma nafasi nyingi za maamuzi katika nyanja za kisiasa, kijamii na kiuchumi zilikua zikiongozwa na wanaume pekee hali iliyosababisha wanawake kuwa nyuma kimaendeleo hivyo kupelekea Mashirika mbalimbali ya kupigania haki sawa kwa wote kuanza harakati za kuwafanya wanawake wajitambue na kufahamu umuhimu wao.
“hivi sasa wanawake wameelimika na wana kila sababu ya kuwa viongozi katika ngazi mbalimbali za serikali na Taasisi zisizo za Kiserikali ndani na nje ya nchi kwa sababu wana uwezo wa kutoa mawazo chanya yenye kuleta maendeleo, pia ni jambo la kufurahisha kuona jamii imekubali mabadiliko haya kwa kuwaruhusu wanawake wapaze sauti zao katika utatuaji wa changamoto mbalimbali zinazoikabili Serikali na wananchi kwa ujumla,” alisema Mhe. Mama Anna.  

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...