Katibu
wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo Chadema Kanda ya Ziwa, Meshack
Micus (kulia), akizungumza juzi kwenye semina kwa viongozi wa Mabaraza
ya Chadema Wilaya ya Nyamagana mkoani Mwanza.
Lengo
lilikuwa ni kuimarisha mabaraza hayo kwa ajili ya utendaji kazi wake
ikiwemo kuhakikisha wanachama wapya wanaendelea kujiunga na chama
chadema ili kukifanya kuendelea kuwa chama cha upinzani chenye nguvu
nchini.
Chama
hicho kililaani zoezi la kuwahamisha machinga kutoka katikati ya Jiji
la Mwanza huku mazingira rafiki yakiwa bado hayajaandaliwa ambapo Micus
alisema hatua hiyo inaweza kusababisha vijana na akina mama wengi kukosa
mwelekeo wa kujitafutia kipato kwa njia sahihi ambapo walihimiza
machinga hao kutengenezewa mazingira bora ya kufanyia biashara zao.Na
BMG Habari
Baadhi
ya viongozi wa mabaraza ya Chadema wilayani Nyamagana wakimsikiliza
Katibu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo Chadema Kanda ya Ziwa,
Meshack Micus (kulia), wakati akizungumza kwenye semina kwa viongozi wa
Mabaraza ya Chadema Wilaya ya Nyamagana mkoani Mwanza.
Diwani
wa Kaya ya Butimba, John Pambalu, akizungumza juzi kwenye semina kwa
viongozi wa Mabaraza ya Chadema Wilaya ya Nyamagana mkoani Mwanza.
Baadhi
ya viongozi wa mabaraza ya Chadema wilayani Nyamagana wakimsikiliza
diwani wa Kata ya Butimba, John Pambalu, wakati akizungumza kwenye
semina kwa viongozi wa Mabaraza ya Chadema Wilaya ya Nyamagana mkoani
Mwanza.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...