Baadhi ya wauguzi wa Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH), leo wametoa zawadi mbalimbali kwa wagonjwa waliolazwa katika hospitali hiyo.
Akizungumza katika hafla hiyo fupi, Mkurugenzi wa Uuguzi katika hospitali hiyo, Bi. Agnes Mtawa amewashukuru wauguzi hao kwa kuonyesha ushirikiano katika kazi na kutoa huduma nzuri kwa wagonjwa.
Mtawa aliwaasa wauguzi kuendelea na upendo huo waliouonyesha katika kipindi chote cha mwaka 2016 kwa kuwa ndio upendo ambao Mungu anataka wauonyeshe kwa wagonjwa.
 Pia, aliwapongeza kwa kukabiliana na changamoto mbalimbali katika mwaka huu na kuwataka kutumia changamoto hizo kama sehemu ya mikakati ya mwaka 2017.
Naye Meneja wa Jengo la Watoto, NPC One, Bi. Anna Mponeja aliwashukuru wauguzi kwa kutoa huduma nzuri kwa wagonjwa katika kipindi chote cha mwaka 2016. Hafla hiyo imeudhuriwa na zaidi ya wauguzi 70. 
 Mkurugenzi wa Uuguzi katika Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH), Agnes Mtawa akizungumza na wauguzi baada ya wauguzi hao kutoa zawadi kwa wagonjwa waliolazwa katika hospitali hiyo. Zawadi hizo zimepokelewa na mtoto Neema Selemani kwa niaba ya wagonjwa wengine. Kutoka Kushoto ni Mkuu wa Jengo la watoto, NPC One,  Bi. Anna Mponeja na Katibu wa Tughe Tawi La Muhimbili, Bw. Faustine Fidelis.
 Mkuu wa Jengo la Watoto, NPC One, Bi. Anna Mponeja akimkabidhi Mkurugenzi wa Uuguzi katika hospitali hiyo, Bi. Agnes Mtawa zawadi maalamu.
 Bi. Anna Mponeja akimlisha keki mtoto Neema Seleman Leo katika hospitali hiyo.
Ni wakati wa kufungua Champainge..Picha zote na John Stephen, Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH). Kwa picha zaidi BOFYA HAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...