Mkaazi wa Singida Mjini, Mrisho Joseph mwenye umri wa miaka 23 ameibuka mshindi baada ya kubashiri vyema matokeo ya mechi kupitia Kampuni ya m-Bet na kujishindia zaidi ya Shilingi Milioni 50/-. 
Mrisho amekabidhiwa fedha zake leo katika hafla  fupi iliyofanyika jijini Dar es Salaam kwenye ofisi za m-Bet 
Kwa upande wake, Mkurugenzi wa m-Bet, Dhiresh Kabba alisema kuwa Kaungame alifanikiwa kuzoa kitita hich baada ya kufanikiwa kutabiri matokeo ya mechi 15 za ligi ya Ulaya kwa mtindo wa kucheza kawaida.
“Tunafarijika kumkabidhi Mrisho Joseph kitita hicho cha Sh milioni 50/- akiwa ndiye mshindi wa m-Bet ambapo amesema atawekeza katika biashara zake ili aweze kusaidia wakazi mbalimbali wa mji wa singida wanaomzunguka,” alisema Kabba.
Aliwataka watanzania kuchangamkia kutumia mtandao wa intaneti kuonyesha ushabiki halisi wa soka akisema kuwa Perfect 12 ni mchezo wa ziada unaoruhusu kutabiri mechi 12 kwa Tsh 1,000 tu ambapo ukipatia zote  unaondoka na kitita chako mchana kweupe na ndicho Mrisho alichofanya. 
Naye Mshindi huyo, Mrisho Joseph amewashauri watanzania wote hasa wakazi wa Singida wenye umri unaoruhusiwa kisheria kujitokeza kubashiri matokeo ya mechi mbalimbali kupitia Kampuni ya m-Bet . 
"Nashukuru sana m-Bet kwa kuniwezesha kujikwamua kimaisha, nitatumia fedha hizi kutimiza ndoto yangu ya kununua kiwanja na kuanza ujenzi", alisema Mrisho.
 Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Michezo ya Kubahatisha Tanzania, Abbas Tarimab (kushoto) akikamkabidhi mfano wa hundi  yenye thamani ya zaidi ya shilingi Milioni 50/- mshindi wa M-bet, Mkazi wa Mkoa wa Singida,Mrisho Joseph(kulia)kwenye hafla fupi ya makabidhiano hayo yaliyofanyika jijini Dar es Salaam leo,Katikati ni Mkurugenzi wa M-bet, Dhiresh Kaba.
 Mkurugenzi Mkuu wa  Bodi ya Michezo ya Kubahatisha nchini, Abbas Tarimba(kushoto)na Mkurugenzi wa M-bet, Dhiresh Kaba,wakimpongeza kwa kumpigia makofi mshindi wa M-bet, Mkazi wa Mkoa wa Singida,Mrisho Joseph(kulia)wakati wa  hafla fupi iliyofanyika jijini Dar es Salaam ya kumkabidhi hundi yenye thamani ya zaidi ya shilingi Milioni 50/- mshindi huyo leo.
Mkurugenzi wa M-bet, Dhiresh Kaba(kushoto)na mshindi wa M-bet, Mkazi wa Mkoa wa Singida,Mrisho Joseph(kulia) wakimsikiliza Mkurugenzi Mkuu wa  Bodi ya Michezo ya Kubahatisha nchini, Abbas Tarimba,akifafanua jambo kwa waandishi wa habari(hawapo pichani) wakati wa  hafla fupi ya kumkabidhi hundi yenye thamani ya zaidi ya shilingi Milioni 50/- mshindi huyo jijini Dar es Salaam leo.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...