WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa anatarajiwa kuwa mgeni rasmi kwenye Siku
ya Maulid ya kuzaliwa kwa Mtume Muhammad (S.A.W) ambayo kitaifa
itaadhimishwa mkoani Singida.
Katibu wa Bakwata Mkoa wa Singida, Alhaji Buruhani Mlau alisema
sherehe za Kitaifa za Maulid ya Mtume Mohammad (SAW) kwa mwaka huu
zinatarajiwa kufanyika Mkoani Singida katika Kijiji cha Shelui,
wilayani Iramba, Singida.
Wiki iliyopita, akitangaza utaratibu wa sherehe hizo, Mufti wa
Tanzania, Sheikh Abubakar Zubeir alisema kwa mwaka huu, Maulid
itasomwa usiku wa Desemba 11 na mapumziko yatakuwa siku inayofuata
yaani Desemba 12.
Mufti wa Tanzania aliwataka Waislamu wote nchini waadhimishe Siku ya
Maulid kwa kufanya usafi, kupanda miti na kuchangia damu. “Waislamu
wanatakiwa kutumia siku hiyo kwa kufanya matendo mema na yenye
kumpendeza Mwenyezi Mungu ikiwa ni pamoja na kufanya usafi kwenye
mitaa yao na kuchangia damu ili kusaidia wenye uhitaji huo,” alisema.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...