Sababu ya mtandao, Dunia ni kama kijiji kimoja.Mtandao umekuwa kitu cha muhimu kwenye maisha ya watu wengi sana,mitandao inatufanya tuwasiliane kwa urahisi na ndugu jamaa na marafiki mbalimbali,inatufanya kupata taarifa mapema zaidi kuliko vyanzo vingi vya taarifa vya ‘kizamani’ kama runinga, redio na magazeti,mitandao pia ni chanzo cha ajira kwa watu wengine.
Hapa chini nakupa dondoo kadhaa za kukusaidia walau kujihadhari na hatari ndogondogo ukiwa kama mtumiaji wa kawaida wa mtandao
1.Usisambaze taarifa zako ovyo.
Kuwa makini unapowasiliana na watu katika mitandao ya kijamii,na kuwa makini zaidi linapokuja suala la kumpa mtu taarifa zako nyeti kama akaunti za benki,au password,usidangaanyike na jumbe za kilaghai kama zinazokutaarifu kushinda bahati nasibu,kupata mkopo au mtu anayetaka kukupa dili lakini anataka taarifa hizo akuwekee kiasi fulani cha fedha,asilimia 99 huwa ni matapeli wa mtandaoni
2. Epuka malumbano yasiyo na maana mtandaoni
Moja ya sababu ya kuwa na mitandao,haswa ya kijamii ni kubadilishana mawazo na mijadala mbalimbali lakini kama ilivyo kwa imani tofauti tulizonazo,wakati mwingi mawazo huwa tofauti-wasilisha mawazo yako kwa hoja na sio mihemko,jifunze kukubali kutokubaliana na mawazo ya wengine kama hamjafikia tamati inayoendana,ni sawa kila mtu kuamua kuamini anachoamini.
La pili ni kukaa mbali na wazinguaji wa mtandaoni(Trolls) hawa ni watu ambao aidha hukataa kila kitu kwa ajili ya ubishi tu au hufanya hivyo kutafuta sifa na ‘likes’ kwa kuonekana wanaenda tofauti na mawazo ya wengine,hapa hata ukiwa na hoja za maana ni kazi bure kwani kwao ubishi wa mtandaoni ni kama mchezona zaidi ya yote epuka matusi,kumbuka kuna sheria za mitandao hivyo unaweza kujikuta mikononi mwa dola kwa sababu ya malumbano yasiyo na mantiki.
3. Usisambaze taarifa usizojua chanzo chake.
Umeamka asubuhi umekutana na taarifa kwenye kundi la WhatsApp mtu fulani maarufu amekufa,bila kuwa na uhakika sana unasambaza kwa makundi yako mengine 8 na jamaa zako kadhaa kwenye simu yako.Unakosea,mtandao ni kama bahari kubwa sana ya taarifa zipo taarifa za ukweli,za uongo za utanina kadharika,na kwa kukusaidia tu kama hujui kuna baadhi ya blogu na tovuti ambazo ni maalumu kwa ajili ya kuchapisha taarifa za utani/uongo(Mfano huzzlers.com)-NDIO,yaani taarifa zote utakazosoma humo ni za kutunga na kufikirika hivyo unapoona taarifa mpya jiridhishe kuhusu chanzo chake kabla ya kusambaza kwa wengine na kuendeleza upotoshaji.
4. Chunguza mtu unayewasiliana naye.
Kweli mitandao ya kijamii imetengenezwa kwa ajili ya kukutanishwa na marafiki,wale tunaowajua toka zamani mashuleni au wapya,lakini kuwa na utaratibu wa kumfahamu mtu unaejuana nae mara ya kwanza mtandaoni kabla ya kuanza kubadilishana nae taarifa zako muhimu na nyeti,kumtumia picha zako au za familia,kuna akaunti nyingine za mitandao ya kijamii ni za watu wanaotumia taarifa za uongo kuonyesha ni mtu au jinsia fulani kumbe sio hivyo inabidi utumie akili ya kuzaliwa katika kujiridhisha na uhalisia wa mtu unayewasiliana naye.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...