Na Ofisa habari Mufindi
Halmashauri ya Wilaya ya Mufindi imeendelea kustawi katika sekta ya elimu  ambapo tathimini ya  matokeo  ya darasa la saba ya Halmshauri hiyo   yanaonesha kupanda kutoka asilimia 80.39 mwaka 2015  hadi  asilimia 84.90% mapema mwaka jana, ikiwa ni sawa na ongezeko la asilimia 4.51.

Akisoma taarifa wakati wa kikao cha thathmini ambacho huwakutanisha wakuu wa shule zote za msingi na maaofisa elimu kata, Ofisa elimu taaluma wa Halmshauri ya Wilaya ya Mufindi Miriamu Ngala amebainisha kuwa tathimini ya ufaulu huo umejumuisha shule 143, watahiniwa elfu 05 mianne 38 ambapo wavulana ni elfu 02 miatatu 84 na wasichana ni elfu 03 na 54 huku wanafunzi waliofaulu na kuchaguliwa kuendelea na elimu ya Sekondari  wakiwa ni 4,617 sawa na asilimia 84.9.
 Mkuu wa Wilaya ya Mufindi Mhe. Jamhuri William katika picha ya pamoja na  na waalimu wakuu wa shule zilizofanya vizuri na kutunukiwa vyet na Fedha 
 Mkuu wa wilya ya Mufindi Mhe. Jamhuri William (kushoto) akitunuku chet na Fedha kwa mmoja kati ya waalimu wakuu ambao shule zao zimefanya vizuri.
Walimu wakuu na maofisa elimu kata wakiimba wimbo wakati wakimlaki mgeni rasmi kwenye ukumbi wa Halmshauri  ya Wilaya ya Mufindi.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...