Captain  Denis Mshami wa wakala wa ndege za serikali napenda kuwashukuru wote kwa upendo na faraja mlioonesha wakati wa msiba pamoja na arobaini ya mke wangu mpenzi Husna Kiluvia Mshami.

Kwa moyo wa dhati kabisa mimi na familia yangu tunapenda kusema asante sana na Mwenyezi Mungu atawajazia pale patapopungua.

Ni watu wengi sana wa kuwashukuru lakini baadhi ya hawa wachache iwe ni uwakilisho wa wengi waliotufariji pamoja na kumuuguza Husna.

Nao ni madaktari ya Hindu Mandal, Dar Group Hospital, Dr Mvungi, Ofisi ya Rais Tume ya Utumishi, Wakala wa Ndege za serikali chini ya Capt. Raymond Musingi, Michuzi blog, majirani pamoja na ndugu jamaa na marafiki. Tunapenda kusema tena asante sana.
Husna, leo ni tarehe 7.01.2017 umetimiza miezi miwili toka uondoke. Nilikupenda sana na nitakupenda siku zote. Mwenyezi Mungu akupe pumziko la amani. Amina.
"Wote wamwaminio Mungu watatambua ukweli wake;wote walio waaminifu watakaa upande wake kwa upendo, maana huwajalia neema na huruma watakatifu wake. Na huwaangalia kwa wema hao aliowateua".
(Hekima ya Sulemani 3:9)

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...