Na Lawrence Raphaely-Bunge.
Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Job Ndugai amewaahidi Viongozi wa Chama cha Skauti Tanzania ushirikiano katika utekelezaji wa shughuli mbalimbali za chama hicho ikiwemo maadhimisho ya Siku ya Skauti Afrika na Maadhimisho ya miaka mia moja ya Skauti hapa nchini.
Mhe Spika aliyasema hayo wakati alipokutana na kuzungumza na Viongozi wa Kamati ya Utendaji ya Skauti Tanzania Ofisini kwake Jijini Dar es Salaam ambao walimuomba awaunge mkono katika shughuli zao.
Spika Ndugai aliwaeleza Viongozi hao kwamba kwa niaba ya Wabunge wote ameupokea ujumbe huo na atajitahidi sana katika kuhufikisha kwa Waheshimiwa Wabunge.
“Ninawashukuru sana kwa ujumbe huu na niwaahidi kwamba tupo pamoja si katika hili tu bali katika mambo yoyote ambayo mtakuwa mkiyafanya na nawaahidi pia ushiriki wa Waheshimiwa Wabunge katika maadhimkisho hayo,” alisema Mhe Spika.
Awali akimuelezea Mhe Spika kuhusiana na Shughuli mbalimbali za Skauti hapa nchini Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi na Tenkonolojia Mhe Stella Manyanya ambaye aliambatana na Viongozi hao wa Skauti alisema pamoja na majukumu mengine Chama hicho cha Skauti kina kazi kubwa ya kuandaa maadhimisho ya Siku ya Skauti Dunia na Maadhimisho ya miaka mia moja ya Skauti hapa nchini.
Spika
wa Bunge Mhe Job Ndugai akizungumza na Viongozi wa Kamati Tendaji ya
Skauti waliomtembelea Ofisini kwake Jijini Dar es Salaam mapema leo. Wa
pili kushoto kwake ni Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi na Tenkonolojia Mhe
Eng. Stella Manyanya (Mb) na anayefutia ni Mwenyekiti wa Kamati ya
Utendaji ya Skauti Tanzania Balozi Nicholas Kuhanga.
Naibu
Waziri wa Elimu, Sayansi na Tenkonolojia Mhe Eng. Stella Manyanya (Mb)
aliyeambatana na Viongozi wa Kamati Tendaji ya Skauti Tanzania
akimueleza jambo Spika wa Bunge Mhe Job Ndugai wakati walipotembelea
Ofisini kwake Jijini Dar es Salaam.
Mwenyekiti
wa Kamati ya Utendaji ya Skauti Tanzania Balozi Nicholas Kuhanga
akimueleza jambo Spika wa Bunge Mhe Job Ndugai wakati walipomtembelea
ofisini kwake Jijini Dar es Salaam.
Spika
wa Bunge Mhe Job Ndugai (aliyekaa kulia) na Naibu Waziri wa Elimu,
Sayansi na Tenkonolojia Mhe Eng. Stella Manyanya (Mb) katika picha ya
pamoja na Viongozi wa Kamati Tendaji ya Skauti Tanzania mara baada ya
kuzungumza nao Ofisini kwake Jijini Dar es Salaam.
Picha na Ofisi ya Bunge.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...