Waziri
wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais- Muungano na Mazingira Mh. January
Makamba akiwa katika kikao na wawakilishi wa sekta binafsi
wakizungumza kuhusu masuala ya ufanisi katika mchakato wa Tathmini ya
athari za Mazingira. Wa kwanza kulia ni Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa
Rais Profesa Faustin Kamuzora. Kikao hiko kimefanyika katika ukumbi wa
mikutano wa Ofisi ya Makamu wa Rais jijini Dar es Salaam.
Baadhi
ya Wadau wa sekta binafsi waliohudhuria kikao hiko wakiwa pamoja na
Watumishi na Wataalamu toka Ofisi ya Makamu wa Rais na Baraza la
Usimamizi wa mazingira(NEMC) wakimsikiliza Mh. Waziri January
Mkamba(hayupo pichani) wakati wa kikao hiko.
Mmoja wa Wadau toka sekta binafsi za wenye mahoteli, viwanda
na fukwe Bi. Lathifa K. Sukes akichangia jambo katika kikao hiko. (PICHA ZOTE
NA KITENGO CHA MAWASILIANO SERIKALINI OMR)
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...