Picha na Fredy Njeje
Katika kuhakikisha vijana
wanashiriki na kujikwamua katika mambo mbali mbali UNESCO Youth Forum waliandaa semina ambayo ilihusu
vijana kushiriki katika programu mbalimbali za umoja wa mataifa, Kudumisha amani
kutoka ngazi ya vijana na jamii kwa ujumla ambapo Global Peace Foundation
Tanzania walitoa mafunzo juu ya maswala hayo, kuhusu kusoma nje na kuelekezwa
njia mbali mbali za kufanya kazi kwa kujitolea katika asasi mbalimbali za
kiraia.
Akizungumza na vijana hao kutoka
vyuo mbalimbali na wale ambao walimaliza vyuo mwakilishi wa asasi ya Kiraia ya Global Peace Foundation(GPF)
nchini Tanzania Bi. Anna Mwalongo alisema kuwa Global Peace Foundation ni Taasisi
isiyo ya kiserikali,ambayo si ya kidini na haitengenezi faida ya aina yoyote
ile ina makao yake makuu
katika jiji la Washington DC nchini
Marekani na lenye matawi yapatayo 23 duniani kote, yakiwemo mabara ya
Afrika,Ulaya, Asia na Marekani ni “Taasisi hii kwa Tanzania ilianzishwa kati kati ya Mwaka juzi 2015
ambapo pamoja na uchaga wake wameonesha juhudi kubwa katika kuhamasisha amani
nchini kuanzia ngazi ya familia na jamii kwa ujumla.” Alisema Anna.
Aliongeza kuwa Mnamo mwezi wa
saba mwaka 2015 Global peace foundation waliandaa Mkutano mkubwa wa amani uliofanyinka
Zanzibar uliojulikana kwa jina la Global peace Leadership Conference (GPLC
Zanzibar) ambapo mgeni rasmi alikuwa ni Makamu wa pili wa Rais Mh. Balozi Seif
Ali na kuhudhuriwa na marais wastaafu kutoka nchi mbalimbali.
"Kabla ya uchaguzi wa mwaka 2015 walifanikiwa kwa kiasi kikubwa kuendesha
kampeni ya “AMANI KWANZA” ambapo aliwalenga wanawake na vijana kushiriki katika
uchaguzi huo kwa amani, alimalizia kwa kusema kuwa kwa sasa GPF wanampango wa
kupanua wigo zaidi ili kuwafikia watanzania wengi zaidi kueleza mambo
mbalimbali ya amani kupitia kampeni yao ya “VIJANA NA AMANI” " Alisema Anna
Kwa upande wake Mwenyekiti wa
UNESCO Youth Forum Bw. Frank Joash alisema vijana wengi hawana uwelewa wa
program mbali mbali za umoja wa mataifa hivyo waliamua kuwakutanisha ili kuwapa
uelewa ili wapate kujiunga.
Bwana Jackson Oganga akiwa anatoa maelezo kwa vijana jinsi ya kupata 'Scholarship' katika zinazotolewa sehemu mbalimbali.
Mwakilishi wa Asasi ya Kiraia Global Peace Foundation (GPF) Tanzania aliyewakilisha katika Semina hiyo Bi. Anna Mwalongo akielezea kwa kifupi kuhusu Asasi hiyo.
Mshauri wa mambo mbalimbali ya Kijamii na uchumi Bw. Anthony Luvanda akitoa masomo mbalimbali ya namna vijana wanavyoweza kujikwamua na kujitegemea kwa kufanya shughuli mbalimbali.
Baadhi ya vijana wakiendelea kusikiliza kwa makini mambo mbalimbali katika Semina Hiyo


Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...