Na Chalila Kibuda, Globu ya Jamii.

Shirika la maji safi na Taka jijini Dar es Salaam (Dawasco) katika siku ya wanawake duniani  imetoa msaada kwa Kituo cha Kulelea Wazee na Watoto cha Mather Theresia kilichopo Kigogo.

Dawasco imetoa msaada wa mchele, mafuta ya kupikia, Sukari, Sabuni , unga wa mahindi, Nepi za watoto pamoja na chumvi.

Akizungumza na baada kutoa msaada huo Mkurugenzi wa Sheria wa Dawasco, Benadetha Mkandya amesema kuwa  Dawasco wanatoa huduma kwenye jamii hivyo wanawajibu kusaidia wazee kwani ipo siku watakuwa wazee na kwenda kuishi katika kituo hicho.

Amesema Dawasco kutokana na kuthamini kile wanachokipata wanaona katika siku ya wanawake kuweza kusaidia wazee.

Benadetha amesema katika kuadhimisha siku ya wanawake iwe ni sehemu kila mwanamke kuweza kujiamini kwa kile anachokiamini katika kuleta matokeo chanya.

Amesema mwanamke sio mtu ambaye yuko kwa ajili ya kupika bali anaweza kufanya jamii ikawa na mabadiliko katika nyanja mbalimbali
 Mkurugenzi wa Sheria wa Dawasco, Benadetha Mkandya(wa kwanza kulia) akikabidhi msaada kwa Mwakilishi wa Wazee katika kituo cha Mother Theresia  leo katika Maadhimisho ya siku ya wanawake duniani.
  Baadhi wafanyakazi wa Dawasco wakiwavisha nguo wa wazee wa kituo cha mother Theresia leo.
Wafanyakazi wa Dawasco wakiwa kwenye picha ya pamoja na Wazee wa Kituo cha Mother Theresia Kigogo leo.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...