Na Humphrey
Shao, Globu ya Jamii
Mwanamitindo
maharufu nchini,Jokate Mwegelo amewataka watoto wa kike kujiamini,ili waweze
kufikia mafanikio katika maisha hayo kwa kuweka juhudi katika elimu.
Jokate
amesema hayo leo katika maadhimisho ya siku ya Wanawake Duniani alipokuwa
akizungumza na wanafunzi wa kike katika shule ya sekondari ya Manzese jijini
Dar es Salaam
“nataka
niwaambie watoto wa manzese sekondari,siri kubwa ya mafanikio ni kujiamini
lakini usijiamini katika ujinga hivyo mnapaswa kujiamini katika vitu vya msingi
ambavyo vitweza kusaidia jamii yetu kutoka sehemu moja kwenda nyingine”
amesema Jokate.
Kwa upande
wake program meneja wa TAI, Edith James amesema kuwa umefika wakati wa wanawake
kujiamini hasa kwa kupata elimu bora juu ya afya ya uzazi na usafi wa mwili kwa
ujumla hasa wakati wanapokuwa katika siku zao.
Amesema kuwa
taasisi ya TAI imekuwa katika kampeni kwa zaidi ya shule kumi za mkoa wa Dar es
Salaam,kwa kutoa elimu kwa watoto wa kike waweze kupata elimu bora juu ya afya
ya uzazi.
Jokate Mwegelo akipima afya katika zoezi liliondeshwa shule ya sekondari Manzese jijini Dar es Salaam
Picha kwa juu ikionyesha namna Jokate alivyokuwa akizungumza na wanafunzi wa shule ya sekondari ManzeseJokate Mwegelo akipima afya katika zoezi liliondeshwa shule ya sekondari Manzese jijini Dar es Salaam
Daktari kutoka tasisi ya TAHMEF, Victoria Joseph akitoa maelekezo juu ya tasisi yao inavyotoa huduma kwa watoto wa kike mashuleni
Joakate Mwegelo akikabidhi taulo za kike kwa mmoja wanafunzi wa sekondari ya Manzese jijini Dar es Salaam
Mkurugenzi wa kampuni ya Kays Hygiene product Malik Mtui akizungumza na wanafunzi wa shule ya sekondari Manzese.
HABARI ZAIDI BOFYA HAPA


Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...