Na Humphrey Shao, Globu ya Jamii
Mwanamitindo maharufu nchini,Jokate Mwegelo amewataka watoto wa kike kujiamini,ili waweze kufikia mafanikio katika maisha hayo kwa kuweka juhudi katika elimu.

Jokate amesema hayo leo katika maadhimisho ya siku ya Wanawake Duniani alipokuwa akizungumza na wanafunzi wa kike katika shule ya sekondari ya Manzese jijini Dar es Salaam

“nataka niwaambie watoto wa manzese sekondari,siri kubwa ya mafanikio ni kujiamini lakini usijiamini katika ujinga hivyo mnapaswa kujiamini katika vitu vya msingi ambavyo vitweza kusaidia jamii yetu kutoka sehemu moja kwenda nyingine” amesema Jokate.

Kwa upande wake program meneja wa TAI, Edith James amesema kuwa umefika wakati wa wanawake kujiamini hasa kwa kupata elimu bora juu ya afya ya uzazi na usafi wa mwili kwa ujumla hasa wakati wanapokuwa katika siku zao.

Amesema kuwa taasisi ya TAI imekuwa katika kampeni kwa zaidi ya shule kumi za mkoa wa Dar es Salaam,kwa kutoa elimu kwa watoto wa kike waweze kupata elimu bora juu ya afya ya uzazi.
 Jokate Mwegelo akipima afya katika zoezi liliondeshwa shule ya sekondari Manzese jijini Dar es Salaam
 Picha kwa juu ikionyesha namna Jokate alivyokuwa akizungumza na wanafunzi wa shule ya sekondari Manzese
 Daktari kutoka tasisi ya TAHMEF, Victoria Joseph  akitoa maelekezo juu ya tasisi yao inavyotoa huduma kwa watoto wa kike mashuleni
 Joakate Mwegelo akikabidhi taulo za kike kwa mmoja wanafunzi wa sekondari ya Manzese jijini Dar es Salaam
Mkurugenzi wa kampuni ya Kays Hygiene product Malik Mtui akizungumza na wanafunzi wa shule ya sekondari Manzese.

HABARI ZAIDI BOFYA HAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...