Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi Tanzania Jenerali Venance Mabeyo amefanya ziara ya kikazi Mkoani Kagera kukagua maendeleo ya ujenzi wa Kituo cha Afya Kabyaile Wilayani Missenyi kinachojengwa upya na Jeshi la Wananchi Tanzania mara baada ya kuathiriwa na Tetemeko la Ardhi lililotokea Mwezi Septemba mwaka jana.
Mkuu wa Majeshi Jenerali Mabeyo alifanya ziara hiyo Machi 2, 2017 na lengo kuu ilikuwa ni kuona maendeleo ya ujenzi wa kituo hicho mara baada muda alioutoa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. John Pombe Magufuli kuisha mwishoni mwa mwezi Februari mwaka huu 2017.
Rais Magufuli alipofanya ziara Mkoani Kagera Januari 1, 2017 alitembelea eneo la Kabyaile Wilayani Missenyi na kukagua maendeleo ya ujenzi wa kituo hicho cha afya na kuagiza kuwa ujenzi huo uwe umekamilika ifikapo Mwisho mwa mwezi Februari 2017.
Mara baada ya kukagua maendeleo ya ujenzi huo Mkuu wa Majeshi Jenerali Mabeyo akiongea na viongozi wa mkoa na wananchi waliofika kumuona kituoni hapo alisema ameridhishwa na hatua iliyofikiwa katika ujenzi huo, pia alishukuru upanuzi wa majengo kuwa ni manufaa kwa wananchi wa Kabyaile na Wilaya ya Missenyi kwa ujumla.


Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...