Na Karama Kenyunko, Globu ya jamii.

Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu imemuachia huru Mbunge wa Singida Mashariki Tundu Lissu baada upande wa Jamhuri kuomba kumuondolea kesi ya uchochezi.

Hata hivyo mara tu baada ya kuachiwa huru alikamatwa tena akiwa katika viunga vya mahakama hiyo na kupelekwa moja moja katika kituo cha polisi kati.

Kabla ya kukamatwa, Mwendesha Mashtaka wakili wa Serikali Paul Kadushi amewasilisha maombi ya kumuondolea Lissu mashtaka mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Huruma Shahidi.

Kadushi amedai kuwa Mkurugenzi wa mashtaka Nchini (DPP), ameona hana nia ya kuendelea na mashtaka yaliyopo mahakamani dhidi ya Lissu chini ya kifungu cha sheria namba 91(1) cha sheria ya mwenendo wa makosa ya jinai (CPA),

Aidha kwa mujibu wa kifungu hicho kinampa mamlaka DPP ya kumuondolea mashtaka mtuhumiwa kabla ya kusikiliza ushahidi lakini anaweza kukamatwa na kushtakiwa upya.

Hakimu Shahidi amesema kwa kuwa upande wa Jamhuri umeomba kumwondolea mshtakiwa mashtaka na kwamba hawana nia ya kuendelea na keshi hiyo mahakama yake imekubaliombi Hilo.

“Mahakama hii inamuachia mshtakiwa chini ya kifungu cha (91) (1),  kama upande wa Jamuhuri ulivyowasilisha maombi yao dhidi ya mshtakiwa” alisema Shahidi.

Lissu alifikishwa mahakamani hapo mapema February akadaiwa kuwa, Januari 11 mwaka huu alitoa matamshi ambayo yanaweza kuleta uvunjifu wa amani.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...