Waziri
wa Maliasili na Utalii, Professa Jumanne Maghembe(wa pili kutoka
kushoto) akizungumza na wafanyabiashara kwenye mkutano wa majadiliano
kati ya Serikali na Sekta binafsi katika kulinda na kuhifadhi Maliasili
hasa za wanyama pori kwenye ukumbi wa Mwalimu Nyerere jijini Dar
leo.(Picha na Karama Kenyunko wa Blogu ya Jamii)
Mwenyekiti
wa Taasisi ya sekta binafsi nchini (TPSF), Dk. Reginald Mengi
akizungumza na wafanyabiashara pamoja na viogozi juu ya uhifadhi wa
wanayamapori leo kwenye ukumbi wa mkutano wa Mwalimu Nyerere jijini Dar.
katika mkutano huo wafanyabiashara wameahidi kuipatia serikali uwezo
zaidi wa kupambana na ujangili dhidi ya wanyamapori.
Balozi
wa Uhifadhi wanyamapori, Jacqueline Mengi akizungumza kuhusu uzuiaji wa
ujangili kwa wanyamapori kwenye ukumbi wa mkutano wa Mwalimu Nyerere
jijini Dar
Baadhi
ya wadau wakiwa kwenye mkutano wa majadiliano kati ya Serikali na Sekta
binafsi katika kulinda na kuhifadhi Mali asili hasa za wanyamapori.
Waziri
wa Maliasili na utalii, Prof. Jumanne Maghembe akifafanua jambo kwa
waandishi wa Habari mara baada ya kumaliza mkutano wa majadiliano kati
ya Serikali na Sekta binafsi katika kulinda na kuhifadhi Mali asili
hasa za wanyama pori.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...