Na Zainab Nyamka,Globu ya Jamii.

Baada ya kutoka na ushindi wa goli 2-0 dhidi ya Ruvu Shooting katika mchezo wa ligi kuu Tanzana Bara uliopigwa jana katika Uwanja wa Taifa hatimaye uongozi wa klabu hiyo umekata rufaa kwa kadi ya njano aliyopewa mshambuliaji wao Obrey Chirwa kwenye kamati ya masaa 72.

Kadi hiyo aliyopewa Chirwa katika dakika ya 45 ilikuwa ni baada ya kufunga goli linaloleta utata mpaka muda huu ambapo mwamuzi Ahmada Simba alilikataa na kumlima kadi na baadae kidogo kufanya kosa la utovu wa nidhamu na kupatiwa kadi nyekundu.

Uongozi wa Yanga umekataa rufaa hiyo kwenye kamati ya masaa 72 kuhusiana na kadi aliyopatiwa mshambuliaji wao wa kimataifa Chirwa aliyopatiwa katila dakika ya 45 baada ya mwamuzi kulikataa goli alilofunga.

Baadhi ya viongozi wa Yanga waliokuwapo uwanjani walionesha kusikitishwa na tukio la kukataliwa kwa goli ma Chirwa kupewa kadi ya njano na kuamua kukataa rufaa haraka sana.

Viongozi hao, walienda mpaka vyumba vya kubadilishia waamuzi na kumpatia kamisaa wa mchezo huo rufaa hiyo ili iweze kusikilizwa ndani ya masaa 72.

Kwa sasa katika kikosi cha Yanga, Chirwa amekuwa tegemeo kubwa sana akiziba pengo la Mzimbabwe Donald Ngoma aliye majeruhi ya goti kwa takribani wiki tatu sasa.
Mshambulaji wa Kimataifa kutoka Zambia Obrey Chirwa akitoka uwanjani baada ya kuonyeshwa kadi nyekundu kwenye mchezo wa ligi kuu dhidi ya Ruvu Shooting.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...