Makamu
Mkurugenzi Mtendaji wa kampuni ya simu ya Halotel Pham Dinh Quan
(kulia) akiwaongoza wafanyakazi wenzake kutoa zawadi kwa mmoja wa mama
wa watoto wenye vichwa vichwa vikubwa na mgongo wazi waliolazwa Taasisi
ya Mifupa Muhimbili (MOI).
Meneja Mawasiliano wa kampuni ya simu ya Halotel, Stella Pius (kulia) na wafanyakazi wenzake wakitoa zawadi kwa mmoja wa mama wa watoto wenye matatizo ya vichwa vichwa vikubwa na mgongo wazi waliolazwa Taasisi ya Mifupa Muhimbili (MOI)
Wafanyakazi
wa kampuni ya simu ya Halotel wakiwa katika picha ya pamoja nje ya wodi
ya watoto ya Taasisi ya Mifupa ya Muhimbili (MOI) kabla ya kutoa zawadi
ya Pasaka kwa watoto hao.
Wito
umetolewa kwa jamii ya watanzania kuacha mila potofu inayopelekea tabia
ya baadhi ya wazazi kuwaficha watoto wenye matatizo mbalimbali hasa
tatizo la kichwa kikubwa na mgongo wazi bali wawapeleke hospitali mapema
ili wapate matibabu kwani wanaweza kupona endapo wakiwahishwa
hospitali.
Wito huo umetolewa na Afisa Mawasiliano mwandamizi wa Hospitali ya Mifupa (MOI) Bi. Mary Ochieng, wakati akitoa maelezo kwa wafanyakazi wa kampuni ya simu ya Halotel walipotembelea wodi za watoto hao pamoja na kutoa misaada ya kijamii, akizungumza na wafanyakazi hao Ochieng, amesema kuwa licha ya Taasisi hiyo kufanya jitihada kubwa za kutoa elimu na kufanya upasuaji kwa watoto hao bure bado kuna baadhi ya wazazi wameendelea na tabia ya kuwaficha watoto wao.
“Tangu Taasisi yetu ichukue jukumu hili imefanya kazi kubwa sana, kwa kushirikiana na wadau mbalimbali tumeweza kutoa matibabu kwa watoto wengi, ila changamoto kubwa bado inabaki kwa baadhi ya wazazi ambao wanawaficha watoto wao pale inapotokea wakagundua watoto wao wana matatizo ya vichwa vikubwa au mgongo wazi” Alisema nakuongeza.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...