Na Catherine Sungura, WAMJW
Ujumbe wa wawekezaji toka nchini Misri umewasili
nchini kufanya mazungumzo na serikali ya Tanzania kwa nia ya kujenga viwanda vya dawa za binadamu zikiwemo za
majimaji pamoja na zile za antibiotic.
Ujumbe huo ulikutana jana na Waziri wa
Afya,Maendeleo ya Jamii, Jinsia, wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu pamoja na wawakilishi toka wizara
Viwanda,Biashara na Uwekezaji na Kituo cha Uwekezaji cha Taifa (TIC) kwenye
ofisi ndogo ya wizara ya afya, maendeleo ya jamii,jinsia,wazee na watoto
iliyopo jijini Dar es Salaam
Ujumbe huo ulisema kuwa kiwanda
walichokusudia kujenga nchini hapa kitazalisha
dawa za majimaji yaani “IV Fluids” pamoja na “antiobiotics” za aina
mbalimbali ikiwemo "Paracetamol IV”
na dawa za kutibu Malaria
Aidha, walisema lengo lao ni kujenga kiwanda
kikubwa ambacho kitakuwa na uwezo wa kuzalisha dawa ambazo zitawahudumia
watanzania pamoja na nchi za Afrika Mashariki na ya kati. Wawekezaji hao pia wanatarajia
kuisaidia Tanzania katika uzalishaji wa chanjo ya ugonjwa wa homa ya Ini
(Hepatics B na C ).
Kwa upande wake Waziri Ummy amewaahidi
wawekezaji hao kuwasaidia katika mipango ya ujenzi huo na kutoa ushirikiano wa
dhati katika kufanikisha viwanda hivyo vinajenga nchini kwa muda uliopangwa.
“Naelekeza kwa taasisi zote zitakazoguswa na
uanzishwaji wa viwanda hivi watoe ushirikiano wa hali ya juu ili lengo hili
lifikiwe,soko la dawa hapa nchini lipo naomba niwahakikishie hili”alisema
waziri Ummy.
Waziri Ummy aliwaomba wawekezaji hao
kuharakisha ujenzi wa viwanda huo na kujengwa ndani ya miezi kumi na nane kama
walivyoahidi ili watanzania waanze kunufaika mapema.
Waziri wa Afya,Maendeleo ya Jamii, Jinsia, wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu katika mazungumzo na Ujumbe huo wa wawekezaji toka nchini Misri kwenye ofisi ndogo ya wizara hiyo iliyopo jijini Dar es Salaam
Wawakilishi toka wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji na Kituo cha Uwekezaji cha Taifa (TIC) wakiwa katika mazungumzo hayo kwenye ofisi ndogo ya wizara ya afya, maendeleo ya jamii,jinsia,wazee na watoto iliyopo jijini Dar es Salaam
Waziri wa Afya,Maendeleo ya Jamii, Jinsia, wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu katika picha ya pamoja na Ujumbe huo wa wawekezaji toka nchini Misri na Wawakilishi toka wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji na Kituo cha Uwekezaji cha Taifa (TIC) baada ya mazungumzo kwenye ofisi ndogo ya wizara hiyo iliyopo jijini Dar es Salaam
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...