Halmashauri
ya Wilaya ya Handeni imezindua jukwaa la uwezeshaji wanawake kiuchumi
kwa wanawake wa Wilaya ya Handeni kwenye ukumbi wa maount Ilulu uliopo
Kabuku mjini lenye ujumbe wa “Wezesha wanawake kiuchumi ili kujenga uchumi wa kati na Tanzania ya Viwanda”.
Jukwaa
hili linalengo la kuwakutanisha wanawake pamoja na kujadili fursa,
changamoto na jinsi ya kushiriki kikamilifu katika biashara na shughuli
nyingine za kiuchumi katika Wilaya ya Handeni.
Akizungumza kwenye uzinduzi wa Jukwaa hilo Katibu Tawala wa Wilaya ya Handeni Bw.
John Mahali aliyekuwa mgeni rasmi akimwakilisha mkuu wa Wilaya ya
Handeni Mh. Godwin Gondwe alisema kuwa jukwaa la wanawake hilo litasaidia kuongeza uelewa kwa wanawake katika upatikanaji wa mitaji , sheria za nchi katika masuala ya kiuchumi na jinsi ya kujitegemea.
Aliongeza
kuwa wanawake wamekuwa hawapati fursa za kutosha za kiuchumi hapa
Nchini hata na duniani kote kutokana na kutokuwa na usawa katika fursa ,
uwezo wa kupata mitaji.
“jukwaaa
litasaidia kuondoa matabaka na sheri ambazo zitasaidia kupunguza
ubaguzi wa kiuchumi kwa wanawake, ambalo ni jambo la muhimu sana katika
kuleta maendeleo ya usawa katika pato la Taifa, jamii na familia”
alisema Bw. John.
Mkurugenzi
Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Handeni Bw William Makufwe
wakwanza kulia akifuatiwa na Katibu tawala Wilaya Bw John Mahali
wakitazama Moja ya bidhaa ya vikapu vinavyotengenezwa na kikundi cha
wanawake tupendane cha segera
Katibu tawala Wilaya Bw John Mahali akizungumza na wanawake waiojitokeza kwenye Uzinduzi wa jukwaa Hilo.
Mwenyekiti
wa jukwaa la kuwezesha wanawake kiuchumi Wilaya Bi Fatuma Zuberi
akipokea katiba kutoka Kwa mgeni rasmi Katibu tawala Wilaya Bw John
Mahali.
Baadhi ya wanawake wakishiriki wa Uzinduzi wa jukwaa la kuwezesha wanawake kiuchumi Wilaya ya Handeni.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...