Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akisaini Amri ya Rais (Presidential Order) kuifuta   Mamlaka ya Ustawishaji Makao Makuu CDA, tukio lililofanyika Ikulu jijini Dar es Salaam. 

 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza na viongozi mbalimbali wa Serikali akiwemo Makamu wa Rais Samia Suluhu Hassan, Waziri Mkuu Kassim Majaliwa, Waziri wa Ardhi William Lukuvi, Waziri wa Katiba na Sheria Profesa Palamagamba Kabudi, Katibu Mkuu Kiongozi Balozi Mhandisi John Kijazi kuhusu uamuzi wake wa kuifuta   Mamlaka ya Ustawishaji Makao Makuu CDA,tukio lililofanyika Ikulu jijini Dar es Salaam. 
 Viongozi mbalimbali wa Serikali akiwemo Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Jordan Rugimbana wakifatilia kwa makini Hotuba ya Rais Dkt. John Pombe Magufuli mara baada ya kutia saini Amri ya Rais (Presidential Order) kuifuta   Mamlaka ya Ustawishaji Makao Makuu CDADodoma ,tukio lililofanyika Ikulu jijini Dar es Salaam.
 Waziri wa Katiba na Sheria Profesa Kabudi akisoma Rasimu ya Amri ya Rais (Presidential Order) kabla ya Rais Dkt. John Pombe Magufuli kuisaini ili kuifuta CDA Ikulu jijini Dar es Salaam.
  Makamu wa Rais Samia Suluhu Hassan, Waziri Mkuu Kassim Majaliwa, Waziri wa Ardhi William Lukuvi wakifatilia kwa makini wakati Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli alipokuwa akizungumza mara baada ya kuifuta Mamlaka ya Ustawishaji Makao Makuu CDA,tukio lililofanyika Ikulu jijini Dar es Salaam.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa katika picha ya pamoja na Makamu wa Rais Samia Suluhu Hassan, Waziri Mkuu Kassim Majaliwa, Katibu Mkuu Kiongozi Balozi Mhandisi John Kijazi, Waziri wa Ardhi William Lukuvi, Waziri wa Katiba na Sheria Profesa Palamagamba Kabudi, Naibu Waziri Ofisi ya Waziri mkuu, Kazi, Vijana na Ajira Anthony Mavunde pamoja na Mwenyekiti wa CCM mkoani Dodoma Adam Kimbisa mara baada ya kuifuta Mamlaka ya Ustawishaji Makao Makuu CDA,tukio lililofanyika Ikulu jijini Dar es Salaam.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiagana na aliyekuwa Mkurugenzi Mkuu wa CDA Eng. Paskasi Muragili mara baada ya kuifuta mamlaka hiyo Ikulu jijini Dar es Salaam.
 PICHA NA IKULU.


Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...